Ikiwa una Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo au Habari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com.
Laulensi
Masha akiwa na wakili wake Elias Kifunda wakiwa wanabadilishana
mawazo kabla ya kusomewa mashitaka yaliyokuwa yakimkabili ya kufanya
mkutano bila kibali na kuingia kwenye makazi ya wakimbizi bila kibali
Laulensi Masha akiwa na watuhiwa wenzake wakiwa wamefikishwa katika
Mahakama ya Wilaya ya Mpanda kijibu tuhuma zilizokuwa zikiwakabili za
kufanya mkutano bila kibali na kuingia kwenye makazi ya wakimbizi bila
kibali
Picha na Walter Mguluchuma wa Katavi yetu Blog
Na Walter Nguluchuma-Blogs za Mikoa
Aliyekuwa Waziri
wa Mambo ya ndani ya Nchi Laulensi Masha akiwa na viongozi sita wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA) wa Mkoa wa Katavi wamefikishwa
katika Mahakama ya Wilaya ya Mpanda kwa
tuhuma za kufanya mkutano wa hadhara na
kuingia bila kibali kwenye Makazi ya Wakimbizi ya Katumba Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi huku wakiwa chini ya ulinzi mkali wa Polisi
waliokuwa na Bunduki na mabomu ya machozi
Masha na watuhumiwa
wenzake sita walifikishwa kizimbani jana
mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa
Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Chiganga Ntengwa na kusomewa mashitaka na mwanasheria wa kutoka ofisi ya
mwanasheria ya Mkoa wa Katavi Lungano Mwasubila
Watuhumiwa waliosomewa mashita na mwanasheria
wa Serikali ni Laulensi Masha, Gerald Kitabu
mgombea Ubunge wa Jimbo la
Nsimbo(CHADEMA) Abrahamu Mapunda mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya
Mpanda,Fransico Misigalo katibu wa bavicha
wa Mkoa wa Katavi , Sinsilausi
Kaswele Mwenyekiti Chadema wa jimbo la Nsimbo Lameck
Costantino Katibu wa Chadema
jimbo la Nsimbo na Galus Adamu mwanachama wa Chadema
Mwanasheria wa
Serikali Lugano Mwasubila alidai mahakama hapo kuwa Masha
ambae ni mtuhumiwa wa kwanza walitenda kosa hilo hapo oktoba 19 mwaka huu majira ya saaa saba
mchana huko katika Makambi ya Wakimbizi ya Katumba
Watuhumiwa
wanadaiwa walisomewa mashitaka matatu ambapo
kosa la kwanza wameshitakiwa kwa kuingia kwenye makazi ya wakimbizi bila
kibali cha Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi
Shitaka la pili
wameshitakiwa kwa kosa la kufanya mkutano kwenye makazi ya wakimbizi ya katumba
na shitaka la tatu wameshitakiwa kwa kosa la kuingia kwenye kambi ya wakimbizi
wa Katumba bila kibali cha Mkuu wa Makazi ya wakimbizi ya Katumba
Hakimu Chiganga
baada ya watuhumiwa kusomewa mashitaka hayo na mwanasheria wa Serikali
aliwataka watuhumiwa wajibu mashitaka
hayo na watuhumiwa wote saba walikana
mashitaka hayo
Baada ya Masha na watumiwa wenzeke
saba kukana mashitaka hayo mwanasheria wa Serikali Mwasubila aliiomba Mahakama isitowe mdhamana
kwa Laulensi Masha kwa kile alichodai
mahakamani hapo kuwa Masha anakesi nyingine ya jinai katika Makakama ya Kisutu Dares salaam hivyo hatakiwi kupewa dhamana ila watumiwa wengine sita wao dhamana zao
zipo wazi
Mwanasheria
aliyekuwa akiwatetea Masha na wenzake
Elias Kifunda alipinga pingamizi hilo kwa kile alieleza kuwa Masha alifikishwa Mahakamani Kisutu
lakini Mahakama bado haija mtia hatiani hivyo
anayo haki ya kupewa mdhama endapo
kama itatimiza mashariti
Baada ya
mabishano ya kisheria baina ya Mwanasheria wa Serikali na wakili Kifunda yaliodumu kwa dakika 30 Hakimu Chiganga alilazimika kuharisha kesi hiyo kwa
muda wa dakika 40 ili kupitia vifungu vya
sheria walivyokuwa wakibishania wanasheria hao ili aweze kutowa maamuzi
ya kukubali mdhamana wa Masha au kukataa
Hakimu Chiganga
baada ya kupitia vifungu vya sheria
alikubaliana na ombi la
Wakili wa Masha la kupewa mdhamana Laulensi Masha kwa kile aliileza Mahakama kuwa shitaka aliloshitakiwa nalo Mahakama ya Kisutu
alimfanyi MashaMahakama imnyime adhabu kwa kile alieleza kuwa bado shitaka
alinalo alijamtia hatiani
Hivyo Mahakama
iliwapatia mdhamana Masha na
wenzake sita kwa mashariti ya kudhaminiwa na mtu mmoja kwa kila mtuhumiwa kwa kiasi cha shilingi
laki moja kwa kila mtuhumiwa na watuhiwa wote walitimiza mashariti na
kuachiwa
Hakimu Mkazi
Chiganga Ntengwa baada ya watumiwa kutimiza mashariti alihairisha kesi
hiyo hadi Nombe 19 mwaka huu
Na katavi yetu Blog (Blogs za Mikoa)
No comments:
Post a Comment