Shamma Gwajima (kulia) akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) kushoto ni Raphah Gwajima.
Watoto hao wakisikiliza kwa makini maswali kutoka kwa waandishi wa habari kabla ya kuyajibu.
Wanahabari wakiuliza maswali.
Shamma akijibu moja ya maswali ya waandishi wa habari.
Wanahabari wakiuliza maswali.
Shamma akijibu moja ya maswali ya waandishi wa habari.
ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat
Gwajima, ametumiwa waraka mzito na wanaodai kuwa watoto wa kaka yake
Gwajima, Faustine Mathias Gwajima, ambaye kwa sasa ni marehemu,
wakimtaka askofu huyo kumfufua baba yao ndani ya siku 14 la sivyo
watamfikisha mahakamani kwa kile walichokitaja kuwa amewasababishia
athari kubwa za kisaikolojia kwa muda mrefu.
Wakizungumza mapema leo hii na waandishi wa habari Idara ya Habari
Maelezo, Jijini Dar, watoto hao waliojitambulisha kwa majina ya Shamma
Gwajima (18) na Raphah Gwajima (17) walisema kuwa baba yao ambaye ni
kaka wa Askofu Gwajima alifariki dunia mwaka 2008 mkoani Mwanza kwa
maradhi ambapo Askofu Gwajima wanayemwita baba mdogo alifika msibani
hapo na kuwataka ndugu na marafiki waliokuwa wakiomboleza kifo cha
mpendwa wao wasihuzunike kwa kuwa marehemu hakuwa amekufa bali amelala
tu.
“Mchungaji Gwajima alitukataza tusilie na tusihofu kwa chochote kwa
kuwa alikuwa na uwezo wa kumuombea marehemu hadi afufuke. Kauli hiyo
ilitufanya tuanze kufurahi na akaushika mwili wa marehemu katikati ya
umati wa watu na kuanza kuutikisa akimtaka baba yetu aamke lakini
hakuamka,” alisema Shamma.
Watoto hao walidai kuwa tangu siku hiyo Gwajima aliondoka kimyakimya
na kuingia mitini na kudai kuwa jambo hilo limewaathiri kihisia na
kisaikolojia na wanajiandaa kumshtaki kutokana na usumbufu
aliowasababishia katika kipindi kigumu cha msiba wa baba yao.
Watoto hao walienda mbali zaidi na kudai kuwa waliamua kukaa kimya
wakiamini Askofu Gwajima ambaye ni baba yao mdogo anastahili heshima ya
kichungaji mbele za watu, lakini walidai kuwa wanashangazwa na mambo
ayafanyayo hivi karibuni kama vile kuwatukana watumishi wenzake na kutoa
siri za waumini wanaoenda kwake kwa ajili ya kupata huduma za maombezi.
Aidha walidai kuwa Askofu Gwajima ni tapeli kwa kuwa anatumia huduma
ya kufufua misukule ‘hewa’ kwa maslahi yake binafsi na kuitaka serikali
iingilie kati kumchukulia hatua huku wakiitaka jamii isikubali
udanganyifu wa askofu huyo kwa kuwa kama kweli anafufua watu basi
angemfufua kaka yake.
“Je, misukule ambayo anatangaza ameifufua, tujiulize kabla ya
kufariki ilikuwa ikiishi wapi? Na, je, kuna vyeti vya kifo
vinavyothibitisha kama watu hao wanaofufuliwa walikufa kweli? Je, ndugu
wa hiyo misukule wapo?” walisema watoto hao na kuongeza kuwa kutokana na
kushindwa kwake kumfufua baba yao, Gwajima amewatelekeza kwa kutowapa
msaada wowote licha ya yeye kuishi maisha ya kifahari.
(Picha/GPL/Chande Abdallah)
CHANZO GLOBAL PUBLISHERS
No comments:
Post a Comment