Ikiwa una Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo au Habari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com.
Habari
zenu wasomaji wa makala haya, mimi nimeamka salama, bila shaka wasomaji
wangu ni wazima na mnaendelea vema na ujenzi wa taifa hili, kwa
wagonjwa nawaombea heri mtapona.
Tunaelekea uchaguzi mkuu siyo vema nikaanza mada bila kuwakumbusha
kupiga kura ili kumchagua yule unayeona anafaa na kumbuka kupiga kura
ili usije kujutia kuchaguliwa kiongozi na mtu.Wiki hii nimekuja na mada
hii ya mama wakwe wanaopenda kuingilia ndoa za watoto wao ili
kuwakumbusha kuwa si vema mtu akishakuwa na mkewe kufuatiliwa kama mtoto
mdogo.
Siku zote nimekuwa na mada mpya kutokana na ujumbe mnaonitumia na
wengi mmekuwa mkiomba ushauri kupitia mada hizihizi, sasa leo nina
ushahidi wa mwanamke mmoja ambaye yuko kwenye ndoa yake kwa mwaka mmoja
ila kikwazo ni mama mkwe ambaye hupendelea kuwatembelea nyumbani kwao
mara kwa mara.
Hebu msikie mwanandoa huyu analo la kukujuza na kupitia mkasa wake
huenda ukajifunza au wewe mama mkwe mwenye tabia hii huenda ukaiacha
kwani inawezekana hata huna lengo baya lakini hujui kuwa unamkera mkweo.
“Mimi ni mwanamke niliyefanikiwa kuishi kwenye ndoa yangu kwa muda wa
mwaka mmoja, baada ya kuingia kwenye ndoa nilikuwa nahudumiwa na mama
mkwe kwa kila kitu nikajua kwa sababu ya upya wa ndoa yangu kwani hata
nilipowauliza wenzangu waliotangulia kwenye ndoa waliniambia ni kawaida
mpaka zile siku arobaini nikaamua kukaa kimya.
“Kilichosababisha
nikaamua kukwambia Bi Chau ni jinsi mama mkwe wangu anavyonifanyia
mpaka sasa, naona si sawa akija tu nyumbani kwangu naiona nyumba chungu
natamani kuhama mpaka siku anayorudi kwake.
“Kinachonikera zaidi ni jinsi anavyopenda kuingia chumbani kwangu
bila woga na kunipangia niishi vipi na mwanaye wakati tayari tupo kwenye
ndoa, amediriki kunipangia hata matumizi ya ndani kitu ambacho si
sahihi ile ni nyumba yangu na mume wangu.
“Nakumbuka siku moja alimwambia mume wangu kila anachoninunulia na
yeye ampe kama ni kitenge kiwe sare, hivi ni sahihi kweli kuvaa sare na
mama mkwe wangu? Labda niko tofauti naomba unisaidie, kwenye suala la
chakula gani kipikwe nyumbani pia anakuwa mstari wa mbele, nikiamka tu
asubuhi ananiambia leo utapika kitu f’lani hela aachiwe yeye mpaka siku
anayoondoka,” alisema msomaji anayeitwa mama Bahati mkazi wa Kigogo.
Jamani wasomaji hii ni kero ya msomaji mwenzenu kaniletea mezani
nikaona ni bora niwaandikie akina mama wanaojisahau huko mtaani, najua
wapo wengi wa aina hii na leo nimeamua kuwapa funzo dogo tu na nitaanza
kwa kuwauliza.
Hivi mtoto wako akishindwa kuoa si utamaliza waganga wewe?
Wazazi wengi hujisifia na kufurahia kuoa kwa watoto wao wakiwa na
maana kuwa mtoto sasa kakua na akishapata watoto ndiyo kabisa furaha
huwa inakamilika, sasa wewe mzazi unayetamani mwanao kuwa na wewe wakati
wote unamaanisha nini?
Na GPL
Sasa unaikosaje hii nafasi msomaji wangu wa Nguvu ....? usikose kesho
No comments:
Post a Comment