Social Icons

Thursday 22 October 2015

MAGUFULI AENDELEA NA KAMPENI ZAKE JIJINI DAR,APOKELEWA KWA KISHINDO‏

Ikiwa una Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo au Habari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com.

Dk. John Pombe Magufuli Mgombea Urais kupitia CCM akiwanadi wagombea kiti cha Udiwani kwa wakazi wa Kinondoni kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Biafra Kinondoni jijini Dar es salaam.PICHA NA MICHUZI JR-DAR ES SALAAM.
Dk. John Pombe Magufuli akiwahutubia wakazi wa Ubungo.Sinza jijini Dar kwenye uwanja wa TP wakati wa kampeni.Dkt Magufuli ameendelea na kampeni zake mkoani Dar es salaam,ambapo kesho ataendelea kuhutubia kwenye majimbo mbalimbali ya jiji hilo.

Mgombea huyo amefanya mikutano ya kampeni katika majimbo ya Kigamboni, Mbagala, Temeke, Ubungo na Kinondoni huku akiwanadi wagombea ubunge na udiwani wa majimbo hayo, Uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unatarajiwa kufanyika jumapili Oktoba 25 mwaka huu.
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Biafra Kinondoni jijini Dar es salaam.
Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli akiwasalimia baadhi ya wakazi wa mji wa Kigamboni,waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika uwanja wa Machava Kigamboni leo.
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika uwanja wa Machava Kigamboni leo.
Dk. John Pombe Magufuli Mgombea Urais kupitia CCM akimnadi mgombea ubunge jimbo la Kigamboni Dk. Faustine Ndugulile.
Umati wa wananchi waliojitokeza katika mkutano wa kampeni wa CCM kwenye uwanja wa Zakhem Mbagala.
Umati wa wananchi waliojitokeza katika mkutano wa kampeni wa CCM kwenye uwanja wa Zakhem Mbagala.
Furaha inapozidi hakuna wa kuizuiaaa...!
Umati wa wananchi wa Mabagala waishangilai jambo kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika uwanja wa Zakhem Mbagala,jijini Dar
Dkt Jonh Pombe Magufui akiwahutubia wananchi wa Mwembeyaga wilayani Temeke kwenye mkutano wa kampeni kuomba kura wananchi ili apewa ridhaa ya kuwaongoka katika kipindi cha awamu ya tano.
Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli akimnadi mgombea Ubunge jimbo la Temeke,Ndugu Zuberi Abas Mtevu.
Dk. John Pombe Magufuli Mgombea Urais kupitia CCM akipokelewa kwa shangwe na mapambo ya bendera za vyama mbalimbali zilizopambwa kuanzia Ubungo mataa mpaka kituo cha mabasi cha ubungu kufuatia ujio wa mgombea huyo jijini Dar es salaam kwa ajili ya mikutano ya kampeni.
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika uwanja wa TP Sinza katika jimbo la Ubungo jijini Dar es salaam.
Dkt Magufuli akimnadi Mgombea Ubunge wa jimbo la Ubungo Dkt Masaburi
Dkt Asharose Migiro akimwombea kura za ushindo wa kishindi mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika viwanja vya TP,sinza jijini Dar.
Jaji mstaafu Joseph Sinde Warioba akimpigia debe Dk. John Pombe Magufuli kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Biafra Kinondoni jijini Dar es salaam.

Dk. John Pombe Magufuli Mgombea Urais kupitia CCM akiwahutubia wananchi na kuomba kura za ndiyo kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Biafra Kinondoni jijini Dar es salaam
Sehemu ya umati wa wakazi wa Kinondoni na vitongoji vyake wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akiwahutubia wananchi hao na kuomba kura za ndiyo kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika uwanja wa Biafra Kinondoni jijini Dar es salaam

No comments: