Ikiwa una Tukiko lolote au Habari yoyote usisite kutumia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com
Mgombea
ubunge wa Arusha mjini kwa tiketi ya ACT WAZALENDO Ndugu Estomih Malla
amefariki dunia usiku wa leo saa saba Oktoba 9, 2015 katika hospitali ya
KCMC Moshi.
Ndugu
Malla alipelekwa KCMC jana mchana kutokea Hospitali ya St. Thomas
iliyopo Arusha mjini baada ya kulazwa hapo kwa siku mbili kwa sababu ya
kupata tatizo la shinikizo la juu la damu.
Hali
hiyo ilimtokea siku ya tarehe 6/10/2015 mara baada ya kumalizika
mkutano wa kampeni uliokuwa unafanyika Ngaramtoni,ambapo alilalamika
kusikia kizunguzungu na baadae kukimbizwa hospital ya St Thomas ambapo
madaktari wa pale walisema ndugu Malla anasumbuliwa na uchovu na hivyo
anatakiwa kupumzika kwa muda mrefu.
Kwa
mujibu wa Afisa Habari wa Chama Cha ACT Wazalendo, Abdallah Khamis,
ameithibitishia JamiiForums kutokea kwa kifo hicho na kwamba marehemu
alifariki usiku huu wa Oktoba 9, 2015 saa Saba usiku.
Amesema taarifa zaidi zitatolewa baadae baada ya uongozi wa chama hicho kufanya mawasiliano na viongozi waliopo mkoani Arusha.
Sisi sote ni wa mola na hakika kwake sote tutarejea.
No comments:
Post a Comment