Social Icons

Wednesday 21 October 2015

RAIS DK. JAKAYA KIKWETE KUONGOZA KONGAMANO LA KUELEKEA UCHUMI WA KATI IFIKAPO 2025

Ikiwa una Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo au Habari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com.

 Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Kongamano  kongamano la kuchochea uzalishaji mali, Prof.Leonard  Mwaikambo akizungumza na waandishi wa habari juu ya lengo la kongamano ni kutoa fursa kwa watanzania kwa jumla kuelewa malengo na mwelekeo wa taifa letu kufikia uchumi wa kati .
Waandishi wa habari wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Kongamano  Profesa,Leonard  Mwaikambo.

Na Emmanuel  Massaka ,Globu ya Jamii
RAIS Dk. Jakaya  Kikwete   anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kongamano la kuchochea uzalishaji mali katika kuinua kipaato cha mtanzania  wa kawaida kufikia malengo ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 litakalofanyika kesho katika Ukumbi Diamond Jubilei jijini Dar es Salaam.

Hayo ameyasema leo  Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Kongamano  Prof.Leonard  Mwaikambo kongamano hilo litakuwa na watoa maada mbalimbali na wataalam katika sekta ambazo zitafanya kufikia uchumi huo.

Profesa Mwaikambo amesema kuwa wakati huu kutokana na harakati za uchumi kunahitajika wataalam ambao wamebobea kwa kuleta  maendeleo hayo ambayo watanzania  wanayoyataka kwa kukuza kipato.

 Amesema kongamano hilo linagusa nyanja zote katika sera za vyama hivyo ni muda mwafaka wa kujadili masuala ya uchumi ni ya msingi katika ukuza ji kipato kwa wananchi.

Aidha amesema  wanataaluma hao watatoa mchango wao katika maswala ya kijamii na sekta mtambuka , Utawala Bora ,na Mawasiliano ya kielektroniki kwa ukuzaji wa maendeleo watanzania ,Miundombinu ,Afya ,Maji, Elimu pamoja na ujenzi .

Majadiliano yataongozwa na Waziri Mkuu Mstaaf,Jaji Mstaafu,Joseph Sinde Warioba na neno la shukrani litatolewa na Waziri Mkuu,Mstaafu, John Malecela .

No comments: