Ikiwa una Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo au Habari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Kongamano kongamano la kuchochea uzalishaji mali, Prof.Leonard
Mwaikambo akizungumza na waandishi wa habari juu ya lengo la kongamano
ni kutoa fursa kwa watanzania kwa jumla kuelewa malengo na mwelekeo wa
taifa letu kufikia uchumi wa kati .
Waandishi wa habari wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Kongamano Profesa,Leonard Mwaikambo.
Na Emmanuel Massaka ,Globu ya Jamii
RAIS
Dk. Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kongamano la
kuchochea uzalishaji mali katika kuinua kipaato cha mtanzania wa
kawaida kufikia malengo ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025
litakalofanyika kesho katika Ukumbi Diamond Jubilei jijini Dar es
Salaam.
Hayo
ameyasema leo Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Kongamano
Prof.Leonard Mwaikambo kongamano hilo litakuwa na watoa maada
mbalimbali na wataalam katika sekta ambazo zitafanya kufikia uchumi huo.
Profesa
Mwaikambo amesema kuwa wakati huu kutokana na harakati za uchumi
kunahitajika wataalam ambao wamebobea kwa kuleta maendeleo hayo ambayo
watanzania wanayoyataka kwa kukuza kipato.
Amesema
kongamano hilo linagusa nyanja zote katika sera za vyama hivyo ni muda
mwafaka wa kujadili masuala ya uchumi ni ya msingi katika ukuza ji
kipato kwa wananchi.
Aidha
amesema wanataaluma hao watatoa mchango wao katika maswala ya kijamii
na sekta mtambuka , Utawala Bora ,na Mawasiliano ya kielektroniki kwa
ukuzaji wa maendeleo watanzania ,Miundombinu ,Afya ,Maji, Elimu pamoja
na ujenzi .
Majadiliano
yataongozwa na Waziri Mkuu Mstaaf,Jaji Mstaafu,Joseph Sinde Warioba na
neno la shukrani litatolewa na Waziri Mkuu,Mstaafu, John Malecela .
No comments:
Post a Comment