Ikiwa una Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo au Habari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com.
Naibu
Katibu Mkuu Mpya wa Wizara ya Mawasiliano Sayansi na Teknolojia Ndugu
Emannuel Kalobelo akila kiapo mbele ya Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete
ikulu jijini Dar es salaam leo.
Naibu Katibu Mkuu mpya Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Ndugu Tixon Nzunda akila kiapo mbele ya Rais Kikwete leo.
Katibu
Tawala mpya wa mkoa wa Katavi Mhandisi Madeni Kipande akila kiapo mbele
ya Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es salaam leo na
kukabidhiwa miongozo ya kazi.
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni
Sefue(wapili kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na waliapishwa
keo.Kushoto ni Katbu Tawala Mkoa wa Katavi Ndugu Madeni kipande, wanne
kushoto ni Naibu katibu Mkuu mpya wa Wizara ya Mawasiliano Sayansi na
Teknolojia Ndugu Emmanuel Kalobelo na kulia ni Naibu Katibu Mkuu Mpya
Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma Ndugu Tixon Nzunda.
.(Picha na Freddy Maro).
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo amewaapisha manaibu katibu wawili wa
wizara na Katibu Tawala wa mkoa katika hafla fupi iliyofanyika ikulu
jijini Dar es Salaam.Manaibu katibu walioapishwa ni pamoja Ndugu
Emmanuel Kalobelo anayekuwa Naibu Katibu mkuu Wizara ya Mawasiliano
Sayansi na Teknolojia na ndugu Tixon Nzunda nayekuwa Naibu Katibu
Mkuu,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma.
No comments:
Post a Comment