Social Icons

Monday 19 October 2015

SHINE WITH SHINA ANNUAL GALA 2015 YAFANA GREENBELT, MARYLAND‏

Ikiwa una Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo au Habari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com.
Meza kuu kutoka kushoto ni Bi. Jennifer Jones ambaye ni ni mkuu wa Kamisheni ya wanawake kaunti ya Prince George, Afisa Suleiman Saleh ambaye alimwakilisha Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson Masilingi. Kulia ni Dr. El Senzengakulu Zulu ambaye ndio mwanzilishi na mmiliki wa shule ya Ujamaa inayofundisha tamaduni za bara la Afrika. PICHA NA KWANZA PRODUCTION/VIJIMAMBO BLOG.

Kutoka kushoto ni Dr. John Rutayuga ambaye ni mwanzilish wa Ukwimwi Orphans akiwa meza kuu na Mr and Mrs William.
Mshereheshaji Tuma akifungua pazia ya kuashiria SHINA Gala imefunguliwa rasmi siku ya Jumamosi Octoba 17, 2015 ndani ya Hotel ya Hilton iliyopo Greenbelt, Maryland na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali Watanzania na marafiki zao wakiwemo wawakilishi wa makampuni yanayoshirikiana na SHINA kwa ajili ya kusaidia misaada mbalimbali ikiwemo ujenzi wa shule nchini Tanzania. 
 Kikundi cha sanaa cha Taratibu Youth Association kikifungua pazia la burudani hku wakishangilia muda wote kwa umahiri wao wa kucheza ngoma za asili kutoka Tanzania. Kundi hili hupata mialiko mabara mbalimbali kujifunza na kufanya maonesho ya ngoma za asili ambazo hua kivutia kwa watazamaji.
 Wapiga ngoma wa Taratibu Youth Association.
Mwanzilishi na mmiliki wa SHINA kwa heshima na taadhima akiwashukuru watu waliofika kwenye SHINA Gala Dinner na kusaidia kuchangisha pesa za kusaidia misaada mbalimbali ikiwemo ujenzi wa shule nchini Tanzania.
 Afisa Suleiman Saleh akimwakilisha Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson Masilingi ambaye ndiye aliyekua awe mgeni rasmi kwenye SHINA Gala iliyofanyika siku ya Jumamosi Octoba 17, 2015 katika hoteli ya Hilton, Greenbelt, Maryland nchini Marekani.
Afisa wa Ubalozi Bwn. Suleiman Saleh akimzawadia Bi. Jessica Mushala zawadi kutoka Zanzibar ambayo baadae ilifanyiwa mnada ili fadha zisaidie kumalizia ujenzi wa shule nchini Tanzania.
Bi. Jennifer Jones Kamisheni ya wanawake kaunti ya Prince George's ambaye ndiye aliyekua msemaji mkuu huku akishangiliwa muda wote kwa ujumbe mzito aliokua akiutoa mara kwa mara kwenye hotuba yake.
Bi. Jessica Mushala akimzawadia Bi. Jennifer Jones zawadi maalum.
Bwn. Amos Mushala akimzawadia Dr. John Rutayuga zawadi maalum kutambua mchango wake katika kuendelea kupambana ikiwemo kuwasaidia waathirika wa Ukimwi nchini Tanzania.
Dr. John Rutayuga akitoa shukurani zake kwa SHINA.
Mwimbaji wa nyimbo za injili DMV Bi. Rose Kachuchuru akiimba moja ya nyimbo zake.

Mwambata wa Jeshi Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani na Canada Colonel Adroph Mutta katika picha na mkewe walipohudhuria SHINA Gala Dinner hiyo. 
Kwa picha zaidi bofya HAPA

No comments: