Social Icons

Saturday 31 October 2015

LEO KATIKA MAHUSIANO: MAPENZI YA KWELI YAPO, KUUMIA TUNAJITAKIA , SOMA HAPA UPATE SOMO

Ikiwa una Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo au Habari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com.


Kwanza kabisa nianze kwa kusema kuwa mapenzi ni kitu kizuri kilichoumbwa kwa kila kiumbe chenye jinsia. 
Kwa wanadamu mapenzi huwa ya kipekee zaidi kiasi kwamba kila mmoja amekuwa na tafsiri yake lakini hakuna hata moja inayoweza kujikamilisha kuelezea kikamilifu kabisa maana ya neno mapenzi japo kuwa katika nyakati tofautitofauti kila mtu ameshawahi ‘ku-experience’ yaani kupitia mapenzi aidha kwa kupenda au kupendwa au kupendana na mtu fulani.

Experience hiyo ambayo kila mtu hupitia kwa kupenda au kupendwa huwa ni hisia nzuri ikiwa tu yule unayempenda na yeye akakupenda na hatimaye mkawa penzini. 
Hapo mtu anaweza akajisikia yupo ulimwengu wa kipekee wenye furaha na raha zisizo na kikomo na zisizoelezeka kwa maneno ya kawaida yenye herufi ‘a-z’.
Lakini hayo yote yanaweza kugeuka na kuwa majuto na maumivu makubwa ikiwa tu mpenzi wako akakusaliti au kukuacha wakati bado unampenda. 
Hapo ndipo utasikia kauli kama vile ‘mapenzi mabaya’ au ‘sitapenda tena’ zikianza na kuwaogopesha wengine kuingia kwenye mapenzi tena kiasi kwamba wapo walioapa kutopenda tena hata kama watu wenye mapenzi ya dhati wakitokea huwaacha wapite bila kujua kuwa wanajikosesha bahati.
Ni wazi kuwa hakuna maumivu makubwa zaidi kama yanayotokana na mapenzi lakini mapenzi yenyewe siyo mabaya kiasi cha kugopwa bali ni mazuri sana kiasi kwamba kama yakifuatwa kwa utaratibu sahihi unaweza ukaenjoi bila kuwa na majuto yoyote.
Wapi tunapokosea?
-Wengi tunakosea kwa kupenda kuwa na wapenzi wazuri wa umbo, sura na hata sauti yaani kifupi wanaovutia ili marafiki wakimtazama wamsifie. Hilo ndilo kosa la kwanza.
-Wengi tunapenda kuwa na mpenzi ambaye anajiweza kifedha, suala linalochagizwa na maisha magumu yaliyopo katika nchi nyingi za kiafrika hasa Tanzania ambapo mtu hushindwa kuwa na mpenzi asiye na uwezo wa kifedha japo kuwa anampenda na kukimbilia kwenye fedha ambapo hata hivyo huwa na penzi la upande mmoja yaani mmoja ndiye anayempenda mwenzake kuliko mwenziye.
Lakini wakati yote hayo yakifanyika Mungu kupitia zawadi hiyohiyo ya mapenzi aliyoitunuku kwenye kile moyo ya mja wake, hubakia palepale ambapo bado kila mtu hujiona mpweke au hajatimia kwa kuishi bila kuwa na penzi la dhati yaani bila kujisikia kupendwa au kupenda.
 
Kikubwa ni kwamba hata kama umeumizwa vipi na mapenzi bado mapenzi ya kweli yapo na kuna mtu yupo ambaye anakutafuta wewe unayehitaji mapenzi ya dhati lakini hamjajuana tu. Achana na kauli za ‘nimpendaye bado hajazaliwa,’ ukweli ni kwamba ameshazaliwa kazi kwako.
Usikose kusoma makala ya ijayo inayosema; MJUE MVULANA MWENYE MAPENZI YA DHATI KWAKO itakayoletwa kwenu kupitia Darasa la Malovee hapahapa Fredy Njeje Blog. Kutoka kwa Daktari wa Mapenzi. Contact: 0653146563.
 
 Inaletwa kwenu na Fredy Njeje Blog

1 comment:

chiskamgabbo said...

p