Social Icons

Monday 16 January 2012

Hivi ndivyo Mabucha ya wenzetu yalivyo wanauza kila kitu hakuna kutupa ,,

 Huu ni Mkia wa Mbuzi ambao umenona sana na kwa bei yake ya kilo moja ni Tsh: 15,000 na watu wanavamia sana 
 Kichwa cha Moo kikiwa Dukani Ambapo pia watu wanakuwa wengi sana kutaka kununua  
 Hii ni Baadhi ya minofu iliyo katwa katwa ambapo mteja anachagua vipande anavyo taka anapimiwa kwa kilo kisha anaondoka zake
 Hii ni   mashine maalum inayo tumika kukatia Nyama hizo, na mifupa migumu migumu 
 Hawa ni kuku ambao wanangojea kununuliwa katika eneo hilo la soko la jioni wanaonekana ni wengi lakini baada ya masaa kadhaa wote hutoweka kwa kununuliwa 
 Huu ndio Muonekano wa Maduka hayo mbali Mbali ambapo wanauza kila kitu ikiwemo kuku na mengineyo mengi 
 Hapa sasa ni muonekano baadhi ya vitu kutoka kwa kuku kama vinavyo onekana kuna Firigisi, Maini na Miguu ya Kuku hakuna kinacho tupwa hata nyongo ina kazi ingine kwa hiyo nayo inahifadhiwa 
Hizi ni Kongoro za Moo ambazo zipo tayari kabisa kwa ajili ya kuuzwa, zilikuwa zimejaa eneo hilo lakini wadau wamezishambulia 

No comments: