Social Icons

Thursday 22 November 2012

Tuhuma za Rose Ndauka Kuwatapeli Wasanii Wachanga



Habari mpya kutoka kwa Rose Ndauka baada ya kupiga story na mwandishi wa habari hii ni kuhusu skendo za utapeli.....

Mrembo huyu amefunguka na kusema kwamba kumekuwa na madai mengi sana kwamba amekuwa akiitisha usahili kwa wasanii chipukizi na kuwachukulia fedha bila kuwashirikisha katika filamu zake.....

Ndauka alikanusha na kusema kwamba sio habari za kweli kwani anapoita usahili pale mtu anapofanya vizuri anamchukua na kama akifanya vibaya basi anamuelekeza ili siku nyingine atakapoitaji tena aweze kushiriki tena. 

Hayo ndiyo maneno ya Rose Ndauka baada ya kusikia tetesi ambazo zilikuwa zikizungumziwa kwamba anawachukia wasanii chipukizi wa filamu.
PICHA KWA HISANI YA VIJIMAMB BLOG

No comments: