STAA
aliyekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha msanii wa filamu Elizabeth
Michael ‘Lulu’ anapata dhamana, Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ amefunguka
kuwa baada ya kufanikiwa kwa Lulu sasa anahamia kwa msanii mwingine,
Kajala Masanja.
Akizungumza
nje ya Mahakama Kuu jijini Dar baada ya Lulu kuachiwa, Dk. Cheni
alisema kwa sasa anaanza mchakato wa kumsaidia Kajala mpaka ajue hatima
ya kesi inayomkabili.
“Unajua Lulu siyo mtu wa kwanza kumsaidia na mama yake ndiye aliniomba, nilishawasaidia wengi.
Hata
Cloud alipofungwa nilifuatilia mimi na Dude mpaka mwisho, hatukukata
tamaa na kwa Kajala nitafanya hivyo kwa sababu ni mwenzetu jamani,
naamini Mungu anaweza sana na atafanikisha kila kitu,” alisema Dk.
Cheni.
Kajala
anasota Segerea akikabiliwa na kesi ya kuuza nyumba iliyokuwa imewekwa
bondi na serikali kutokana na mumewe kutakatisha fedha haramu.
No comments:
Post a Comment