Leo nimekaaa sana nikawaza hivi mke wangu atavaa shela ya aina gani? maana za kubuluza mie sitaki kabisaa... sasa nashindwa pata jibu kabisa... maana hata yeye hana jibu
eeeh nikasema hiii akasema hana jibu
Nikamwambia na hiii je akasema kama Cindelea hataki
nikamwambia hii hapa vipi akasema ooooh kwa mbeya atapigwa sana na baridiii
Nikasema hapa vipi akasema ...baby mi na mwili wangu katakaa kweli
Nikauliza hiii akasema twende ingine
Na hiii akasema twende ingine
Hapa je ? akasema haina maadili
naHiii.... akajibu mmmh.... labda
Hii je, akasema tuendelee
na Hii.... Akasema tuendeleee ingawa moyoni aliipenda sana
Hapa vipi? alicho nijibu mimi siwezi andika hapa
Na Hii ya Mwisho je? akasema kwamba inawezekana lakini akasema niendelee kutafuta zaidi
Sasa Mdau... na mpenzi wa kusoma Blog hii.... je unasemaje maana nina zoezi la kutafuta shela... na sitaki la kubuluzaa weeee....... any ways hizi ni aina za kisasa za shela mbalimbali fupi ambazo hazina mkia ....
No comments:
Post a Comment