Social Icons

Sunday, 1 November 2015

LEO KATIKA MAHUSIANO: UTAJUAJE KAMA MWANAUME ANAKUTAMANI AU ANAKUPENDA? SOMA HAPA KWA MAKINI

Ikiwa una Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo au Habari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com.

Kuna mambo mengi ambayo kwa upeo wa kawaida unaweza ukaona kuwa mwanaume fulani anakupenda kwa dhati au anakutamani japo kuwa mambo haya kwa kizazi cha sasa yanahitaji akili sana kujua kwa kuwa vigezo vilivyokuwa vikitumiwa na wapenzi wa kizamani siyo kama vya sasa.

Kwa mfano zamani kupima kama mwanaume ana mapenzi ya dhati, mwanamke atampa sharti mwanaume kuwa wasifanye mapenzi mpaka waoane na kweli kidume kinaweza kikasubiri mwaka mzima wakaishia kupiga stori tu.
Kwa siku hizi hali imekuwa tofauti pengine kutokana na utandawazi na usaliti uliokithiri kiasi kwamba ukimwambia mwanaume eti msifanye mapenzi mpaka muoane, mwenzako ataona unamchelewesha japo anaweza akakukubalia usoni lakini moyoni atatafuta mchepuko na kupoozea hamu ingawa kweli anaweza akawa anakupenda kweli lakini uzalendo utamshinda atakuwa anakuzuga tu kama anakusubiri siku ya siku kama ugonjwa utaupata tu humohumo ndani ya ndoa.
Wanaume wengine wanafanya hivyo kwa kuwa wanajua wapo wadada kibao ambao wakiona mwanaume ameonesha kamsimamo kakutaka kuwaoa basi ndiyo anajifanya anamkazia mwanaume huyo kuhusu suala la mapenzi huku kwa wanaume wengine akichepuka kirahisi; mifano ipo kibao.
Wanaume na wanawake wa sasa wameshtuka mtu akiwa na mtuye anataka amdhibiti kiasi cha kumtimizia kila kitu anachokitaka kiasi kwamba asiweze kusaliti, na ndiyo hali halisi ilivyo.
Sasa katika hali kama hiyo kumjua mtu yupi anakupenda kwa dhati au anakutamani kabla hamjafikia hatua ya kufanya mapenzi ukajutia baada ya kujua ukweli wake inabidi uangalie vitu vidogovidogo tu bila kujali mtazamo wake kuhusu suala la mapenzi.
Swali la kujiuliza hapa ni moja tu:
-Je, uhusiano wenu anauweka wazi au ni wa siri?
Ukiona anakwambia ‘ooh mapenzi yetu sitaki mtu ajue, tufanye siri’ hata marafiki zake hataki wajue kimbia huyo mwongo anakutamani japo sikatai kuwa wapo wengine wanaweza wakakuweka mpaka kwenye mitandao ya kijamii lakini baadaye wakaja kuwa wasaliti lakini kosa linaweza likawa lako wewe mwenyewe bila kujua.
Kosa gani hilo? Kutana nami kesho katika mada inayosema MAKOSA YANAYOVUNJA PENZI LAKO BILA KUJUA.

 Imeandaliwa na Fredy Njeje Blog

No comments: