MTU
mmoja aliyejulikana kwa jina la David Igwesa, anayedaiwa ni daktari
feki amekatamatwa katika Hospitali ya Mkoa wa Mwanza, Sekou Toure huku
akiwa amemtapeli mgongwa Sh. 170,000 kwa ajili ya kumfanyia upasuaji.
Daktari
huyo feki amekamatwa leo saa 4 asubuhi katika hospitali hiyo, baada ya
mgonjwa aliyetapeliwa fedha hizo kuanza kudai risiti za fedha alizotoa
kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji.
Mganga
Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk. Bahati Msaki, amesema taarifa za kuwepo
daktari huyo feki zilianza kutolewa na wagonjwa wa hospitali hiyo kabla
ya mgonjwa aliyetapeliwa, Dotto Chibula kutoa taarifa kwa uongozi
husika.
Amesema
kuwa daktari huyo alitiwa mbaroni kufuatia taarifa za kuwepo kwa
daktari huyo feki na kwamba baada ya kumhoji alidai alikwenda katika
hospitali hiyo kwa ajili ya kujifunza mafunzo ya vitendo kitendo ambacho
ni cha uongo kwani uongozi wa hospitali haumtambui.
“Yeye
anadai alikuja hapa kwa ajili ya kujifunza, taarifa zake za kujifunza
sisi kama uongozi tulikuwa hatuna, tunao vijana wengi ambao wametoka
Bugando (Hospitali ya Rufaa ya Bugando) wanaojifunza sasa huyo ametokea
Bungando ipi.
“Kama
uongozi mara nyingi tumekuwa tukitoa matangazo na kuwaeleza wagonjwa
wanapotoa fedha zao wanapaswa kupewa risiti lakini utakuta mgonjwa
anatoa fedha risti hawatoa, tunaomba wateja wote wawe wanaomba risiti,” amesema Msaki.
Msaki
amesema kuwa baada ya kumhoji `tapeli` huyo hakuwa na zaidi cha
kuzungumza licha ya kudai alikwenda hospitalini hapo kwa lengo la
kujifunza hivyo taarifa za kwamba ni daktari katika hospitali hiyo sio
kweli.
Mgonjwa anena
Tungu
Chibula ambaye ni mtoto wa mgonjwa, Dotto Chibula, amesema kuwa awali
kabla ya kutoa fedha hizo kwa daktari huyo feki, alikuwa anakwenda
anamkuta katika wodi namba saba akiwa na daktari wengine.
Amesema
zaidi ya mara tatu tangu afike hospitalini hapo amekuwa akimkuta
daktari huyo feki akiwa na madaktari wengine wa Sekou Toure wakiendelea
na uotaji wa huduma kwa wagonjwa hivyo alimuamini kumpata fedha hizo.
Amedai
kuwa siku ya kwanza daktari huyo alimueleza kwamba ugonjwa wa baba yake
ni mkubwa sana, hivyo kiasi cha fedha lazima kitakuwa kikubwa ambako
alimwambia anapaswa kutoa Sh. 500,000 ndipo afanyiwe upasuaji.
Hata
hivyo amesema kuwa baada ya kutajiwa kiasi hicho cha fedha, ambacho
walikuwa hawana uwezo nacho walimuomba awapunguzie kwani kiasi hicho ni
kikubwa sana, ambako aliwaambia wakatafute fedha kwanza wakirudi
wataongea.
“Siku
ambayo tulirudi (jana) tulikutana nae huyo huyo akatuambia
atatupunguzia atatufanyia Sh. 500,000, ambako tulisema tuna Sh. 170,000,
ambako tulimpatia na kutuambia nakwenda kuwachukulia risiti,” amesema Chibula na kuongeza.
“Pia
kabla ya kumpatia hizo hela alichukua namba yangu ya simu kwamba
atanipigia na muda mfupi baadae akanipigia akaniambia tukutane kwenye
mgahawa wa hospitali nilienda na nikamkuta tukaongea ndipo
tulikubaliana.”
Daktari feki
Kwa
upande wake, daktari huyo feki, David Igwesa, amesema yeye katika
hospitali hiyo hakuwa muuguzi bali alikwenda kwa ajili ya kujifunza huku
akidai ametokea katika chuo kikuu cha Dodoma, hata hivyo alipotakiwa
kuonyesha kitambulisho cha chuo alidai kimepotea.
Igwesa
amesema kuwa yeye tuhuma zinazoelekezwa kwake hausiki nazo na kwamba
tangu zamani alikuwa na ndoto za kuja kuwa daktari kwani huguswa na
matatizo ya watu hususani wagonjwa.
Pia
amesema kuwa katika kipindi chake cha mwezi mmoja katika hospitali hiyo
ameona mambo mengi ikiwemo fedha nyingi wagonjwa wanazotoa zikipita
katika mifuko ya nyuma na kwamba fedha nyingi hazifiki katika mfuko wa
Serikali kwa ajili ya kuchangia pato la Taifa.
“Tangu
niingie katika hospitali hii sasa yapata mwezi mmoja sasa, nimegundua
kuna matatizo mengi, wagonjwa wanalipa fedha za kupatiwa huduma lakini
hazifiki mahala husika, hivyo suala hilo linapaswa kuchunguzwa,” amesema Igwesa.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Justus Kamugisha, alipotafuta kuzungumzia
juu ya suala hilo lilipofikia, simu yake ya mkononi haikuwa hewani.
No comments:
Post a Comment