Social Icons

Tuesday, 5 January 2016

HII NAYO HATARI: UNYANYASAJI, MKE AKATA NYETI ZA MUMEWE KISA CHAKULA.

Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @officialfredynjejeblog Twitter @Fredynjeje

MWANAUME mmoja mkazi wa Igeregere Bugarika jijini Mwanza amejikuta katika wakati mgumu baada ya kukatwa uume wake na mwanamke anayedaiwa kuwa alikuwa ni mpenzi wake.

Mwanaume huyo ambaye jina linahifadhiwa ameripotiwa kukumbwa na mkasa huo siku ya juma mosi wiki iliyopita nyumbani kwake.


Baadhi ya majirani wa mwanaume huyo wamesema mwanamke aliyefanya tukio hilo alikuwa amelewa na sababu za ugomvi huo ni chakula. BOFYA PLAY KUSIKILIZA MKASA.


Siku ya tukio mwanaume huyo alifika nyumbani kwake akiwa amechoka akitokea shamabi alikokuwa amekwenda kulima.

Baada ya kufika nyumbani hakumkuta mwanamke huyo ambapo aliamua kupika na kumuachia chakula kidogo mwanamke huyo.

Mwanamke anayetajwa kufanya tukio hilo akiwa amezungukwa na majirani chini ya ulinzi na pembeni ni jembe dogo ambalo alitaka kufanya ukatili zaidi.
Muda mfupi baadaye mwanamke huyo alifika akiwa amelewa na kudai chakula na baada ya kubaii hakikuwa kinatosha ndipo alipoamua kuzua ugomvi uliopelekea kupoteza fahamu kwa mwanaume huyo na kisha mwanamke huyo kupata nafasi ya kumkata uume mwanaume huyo kwa kisu.

Mwenyekiti wa mtaa huo Dankani Nyamgonja amesema matukio ya aina hiyo yanapaswa kukemewa kwa nguvu kubwa kwa kuwa yanaondoa utu.


Jitihada za kuzungumza na jeshi la polisi ili kufahamu hatua zilizochukuliwa hadi hivi sasa bado zinaendelea.

CHANZO G SENGO BLOG

No comments: