Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @officialfredynjejeblog Twitter @Fredynjej
Mwalimu raia wa
Kenya ambaye alisifiwa na kuitwa shujaa wakati Waislamu waliwakinga
abiria Wakiristo wakati wa shambulizi la al-Shabab kwenye basi moja
kaskazini mashariki mwa nchi hiyo, ameaga dunia wakati akifanyiwa
upasuaji kutibu majeraha yake.
Salah Farah ambaye alikuwa naibu
mwalimu mkuu katika shule moja ya msingi mjini Mandera, alipigwa risasi
wakati yeye na wenzake walipokataa agizo la wanamgambo wa Kiislamu
waliowataka abiria kugawanyika kwa makundi mawili ya Waislamu na
Wakristo.
Ujasiri wa abiria Waislamu ambao walikaidi agizo la
wanamgambo la kuwataka wajitenge la sivyo wauawe wote ulisambaa kote
duniani wakati habari kuhusu shambulizi hilo ziliporipotiwa tarehe 21
mwezi Disemba.
Mwili wa bwana Farah umesafiriswa kwenda mji wa Mandera tayari kwa mazishi.
BBC Swahili
No comments:
Post a Comment