Social Icons

Monday 29 February 2016

239 KUTOA USHAHIDI KATIKA KESI YA KUPINGA MATOKEO YA USHINDI WA MBUNGE JIMBO LA VWAWA MBOZI MKOANI SONGWE

Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje



WATU 239 watatoa ushahidi katika kesi Namba 6 ya 2015 ya kupinga matokeo yaliyompa ushindi Mbunge wa Jimbo la Vwawa wilayani Mbozi mkoani Songwe, Japhet Hasunga wa CCM.
Kesi hiyo ilifunguliwa na aliyekuwa mgombea wa Ubunge wa jimbo hilo kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka jana kupitia Chadema, Fanuel Mkisi.

Mashahidi hao wataanza kutoa ushahidi Machi 7 mwaka huu. Upande wa mlalamikaji utakuwa na mashahidi 74 na kwa mshitakiwa ni mashahidi 85 huku upande wa Jamhuri wakiwa 80.
Wakili wa mlalamikaji, Boniface Mwabukusi alidai mbele ya Jaji Wilfred Dyansobera wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, alisema katika shauri hilo atawaleta mashahidi 74 kwa ajili ya kutetea hoja za maombi ya mteja wake.
Wakili Sambwee Shitambala anayemwakilisha mlalamikiwa, Mbunge Hasunga, pia alisema anao mashahidi 85.
Aliomba Mahakama wasitajwe majina yao mahakamani, badala yake watakuwa wakitajwa mara tu wanapohitajika.
Kwa upande wake Wakili Mkuu wa Serikali, Joseph Pande aliiambia mahakama kuwa upande wa Jamhuri utakuwa na mashahidi 80 ambao watafika mahakamani hapo kutoa ushahidi wao.
Jaji Dyansobera aliziasa pande zote kuwa mahakama imezingatia kuwa kesi za uchaguzi zimewekewa muda maalumu wa kuzisikiliza chini ya kifungu cha 115 cha sheria ya uchaguzi kuwa kesi hizo zinapaswa kumalizika ndani ya miezi 12.
Chanzo Gazeti la Habari leo

No comments: