Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @officialfredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
Na Lilian Lundo - Maelezo
Msanii
wa Filamu na Balozi wa kutetea watoto waishio katika mazingira magumu
Salma Jabu (Nisha) ameiomba Serikali kuwaangalia watoto hao kwa jicho la
tatu.
Nisha
aliyasema hayo wakati akikabidhiwa ubalozi wa kudumu wa kutetea watoto
waishio mazingira magumu wa New Hope Family Group leo jijini Dar es
Salaam.
“Watoto
hawa wamekuwa rafiki zangu kwa muda mrefu, nimekuwa na huruma sana pale
nilipowaona wanalala na njaa wakati watoto wengine wanakula na kusaza,”
alisema Nisha.
Nisha
aliongeza kwa kusema ni wakati wa kuwafuta machozi na wao wajione ni
moja ya jamii ya kitanzania, kwa yoyote mwenye nguo tatu basi nguo moja
atoe kwa ajili ya watoto hao.
Pia
muigizaji huyo ameiomba Serikali kuangalia watoto hao kwa jicho kubwa,
kwani yapo mengi ambayo wanahitaji ikiwa pamoja na elimu ili waweze
kujiepusha na makundi mabaya ya mitaani.
Kwa
upande wa Mwenyekiti wa New Hope Family Omary Kombe alisema si jambo la
busara kumwita mtoto majina kama panya rodi na mbwa mwitu huku
tukihubiri amani na upendo kwenye majukwaa ya siasa na nyumba za ibada.
Aidha,
Kombe amesema kuwa, familia ya New Hope imemchagua Nisha kuwa Balozi
wao kutokana na moyo wake wa upendo na huruma si tu kwa watoto waishio
katika mazingira magumu bali kwa jamii ya watu maskini na wanyonge.
No comments:
Post a Comment