Social Icons

Tuesday 16 February 2016

HABARI MPASUKO: Mkurugenzi Mkuu Bodi ya Mikopo na wengine watatu wasimamishwa kazi

Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje


Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako amewasitishia mikataba ya kazi Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mikopo (HESLB), George Nyatega na Wakurugenzi wengine watatu kutokana na utendaji mbovu katika kuendesha bodi hiyo.


Wengine ni Mkurugenzi Mkuu wa Mikopo ya wanafunzi asimamishwa kazi, wengine ni Mkurugenzi wa Urejeshaji wa Mikopo, Mkurugenzi Upangaji na Utoaji wa Mikopo.

Mkataba wa Mkurugenzi Mtendaji HESLB umesitishwa. Ilikua uishe mwezi August 2016. Mhasibu Mkuu (Bw. Kisare), Mkurugenzi wa Utoaji Mikopo (Bw. Laizer) na Mkurugenzi wa Urejeshaji Mikopo (Bw. Chagonja) wamesimamishwa kupisha uchunguzi.

Amewateua wafuatao ku Kaimu nafasi; Kaimu Mkurugenzi Mtendaji mteule ni Bw. Jerry Sabi kutoka Mzumbe University na Kaimu Mhasibu Mkuu mteule ni Bw. Daniel Mafie kutoka NECTA

CHANZO: MICHUZI BLOG.


No comments: