Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @officialfredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
Baadhi ya Wanachama wa Chama cha Maadili na Uwajibikaji (CM-TANZANIA) wakimsikiliza Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa nchini wakati wa kukabidhiwa rasmi cheti cha usajili wa muda wa chama chao. |
Na. Jonas Kamaleki.
VYAMA vya Siasa nchini
vimeaswa kuepukana na migogoro na kutumia vikao vyao katika kuendeleza shughuli
zao za kisiasa.
Hayo yamesemwa leo na
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Mhe. Jaji Francis Mutungi wakati akikabidhi
Cheti cha Usajili wa muda kwa Chama kipya cha Maadili na Uwajibikaji
(CM-TANZANIA).
Aidha, Jaji Mutungi
amevitaka Vyama vya siasa nchini kufanya siasa na sio uanaharakati kwaki kwa
kufanya hivyo malengo yao yatatimia na kuifanya Tanzania kuwa na amani.
‘’Msipende kukimbilia
kwenye vyombo vya habari mnapokuwa na migogoro bali malizeni tofauti zenu ndani
ya vikao vyenu kulingana na Katiba ya Vyama vyenu’’, alisema Jaji Mutungi.
Aliongeza kuwa,
Tanzania inapaswa kuwa na vyama vya siasa vinavyojitambua na vinavyojua wajibu
wao katika kuleta maendeleo ya Taifa kwani siasa sio chuki wala uasama.
Kwa upande wake,
Mwenyekiti wa Chama cha Maadili na Uwajibikaji (CM-TANZANIA) Bwana Laban Nkembo
amesema kuwa, chama hicho kimeanzishwa kwa lengo la kuiweka Tanzania kimaadili
na uwajibikaji kwa kuwa kinabeba mambo makubwa mawili yakiwemo Amani na Upendo.
Ameongeza kuwa, chama
chao sio cha Upinzani na kinaheshimu chama kilichopo madarakani hivyo,
kinaahidi kushirikiana na Chama Tawala kuenzi mazuri yanayofanywa na chama
hicho.
‘’Chama chetu sio cha upinzani, tunataka nchi
nyingine duniani ziwe zinakuja kujifunza Tanzania kuhusu amani na maendeleo
tulionayo’’, alisema Nkembo.
Aidha, amebainisha
kuwa, chama chao cha CM-TANZANIA kitatoa ajira za kudumu kwa Wanachama wake na
hata kwa wale wasiokuwa wanachama ambapo kimeshaandaa Idara ya usimamizi mzuri
wa huduma kwa jamii kama vile Wazee, Wajane, Walemavu pamoja na Yatima.
CM-TANZANIA ni Chama
cha 23 kupokea usajili baada ya Vyama vingine vya siasa 22 vyenye usajili wa
kudumu.
No comments:
Post a Comment