Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
(Picha zote na Benedict Liwenga)
Na Benedict
Liwenga.
MUFTI Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakary Zubeiry Bin Ally
amepongeza huduma bora alizopatiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili
Kitengo cha Taasisi ya Moyo cha Jakaya Mrisho Kikwete mara bada ya kupata
ruhusa ya kurejea nyumbani.
Pongezi hizo amezitoa leo Jijini Dar es Salaam mbele ya
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu
pamoja na Viongozi wengine wa Serikali, Viongozi wa Vyama vya Siasa, Viongozi
wa Taasisi mbalimbali, Masheikh, Madaktari pamoja na Waandishi wa Habari waliohudhuria
mkutano Hospitalini hapo.
Mufti Zubeiry ameeleza kuwa, yeye pamoja na Familia yake
pamoja na Baraza la Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) wanatoa shukurani za
dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Joseph
Magufuli kwa msaada wa kumwezesha kupata matibabu hospitalini hapo pamoja na
watu wengine waliofanikisha matibabu hayo kwa namna moja au nyingine.
Amesema kuwa Hospitali hiyo ina Mabingwa wazuri waliobobea
wenye uwezo na endapo wakitumika vizuri hali ya huduma ya afya hospitalini hapo
itavutia kama zile zilizoko nje ya nchi, pia ameiomba Serikali kuona umuhimu wa
kuangalia suala la Madakati, vitendea kazi, pamoja na Wauguzi hospitalini hapo
ili huduma bora zizidi kutolewa.
‘’Namuomba Rais wetu kuitazama Hospitali hii chini ya Wizara
ya Afya pamoja na mabingwa wetu tulionao kwani hapa ni gereji ya binadamu hivyo
panapaswa kuangaliwa kwa makini’’, alisema Mufti Zubeiry.
Katika hatua nyimngine, Mufti Zubeiry amewashukuru Marais
Wastaafu wa Serikali ya Tanzania akiwemo Mhe. Benjamin William Mkapa pamoja na
Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete kwa kufika kumfariji kipindi yuko mgonjwa.
‘’Pia ninawashukuru Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim
Majaliwa Majaliwa na familia yake, Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu,
Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na Naibu Spika Turia Ackson kwa moyo wao wa
kuja kunifariji’’, alisema Mufti.
Kwa upande wake Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu ameeleza kuwa, kwa niaba ya Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, Mhe, John Pombe Joseph Magufuli amezipokea shukurani
hizo toka kwa Mufti Mkuu wa Tanzania kwa kupona na kuruhusiwa hospitalini hapo
na pia amewashukuru Madaktari bingwa na Wauguzi wote walioshiriki katika
kumtibu Mufti huyo.
‘’Mmetupa changamoto sisi ya kutaka kufanya vizuri zaidi, ni
matarajio yetu sisi kama Serikali kuona viongozi wote wa Tanzania akiwemo Mufti
Mkuu na wengine wanatibiwa katika Hospitali yetu ya Taifa ya Muhimbili, hivyo mmetusaidia
sana kutuma ujumbe kwa Watanzania kuwa tunaweza kutumia hospitali zetu katika
kuwatibu viongozi wetu nchini’’, alisema Mhe. Ummy.
Almeongeza kuwa, Wizara ya Afya itaendelea kujitahidi
kuboresha huduma za afya hospitalini hapo, ikiwemo suala la Wataalamu, vifaa
vya tiba pamoja na kuongeza hamasa kwa Watanzania ya kutibiwa hospitalini hapo
kwakuwa Mufti pamoja na baadhi ya na viongozi wengine ambao wamewahi kutibiwa
hospitalini hapo wameonyesha moyo wa kuboresha zaidi huduma hospitalini hapo.
No comments:
Post a Comment