Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
Kamanda
Wa Polisi Mkoani Arusha Liberatus Sabas akionesha moja ya baadhi ya
silaha zilizosalimishwa na wamiliki na nyingine zilizotelekezwa porini.
Bunduki
34 za kivita na za kiraia zilizokuwa zikimilikiwa na wanavijiji wa
Tarafa ya Sale Wilayani Ngorongoro Mkoani Arusha ,zimesalimishwa ikiwa
ni hatua ya kutii agizo la kamati ya ulinzi na Usalama Mkoani humo,
iliyotoa siku saba kwa wananchi wote wanaomiliki silaha kuzisalimisha .
Agizo
hilo linafuatia kutokana na mfululizo Wa matukio ya mauaji ya watu
katika eneo hilo ambao February 21,2016 pekee watu watatu wa Jamii ya
wasonjo waliuwawa kwa kupigwa risasi na watu wanaosaidikiwa kuwa
wafugaji Wa kimasai huko katika kitongoji cha Meje Kijiji cha Kisangiro
Wilayani Ngorongoro,Kamanda Wa Polisi Mkoani Arusha Liberatus Sabas
amesema baadhi ya silaha zilisalimishwa na wamiliki na nyingine
zilitelekezwa porini.
Chanzo : Michuzi Media Group
No comments:
Post a Comment