skip to main |
skip to sidebar
Familia ya pacha wanne yasaidiwa milioni 10 na NMB
-
-
Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Ubungo, Evelyne Mushi (kushoto)
akimkabidhi baba wa watoto pacha wanee, Abednego Andrew Mafuluka mkazi
wa Kimara Mwisho, Dar es Salaam mfano wa hundi ya shilingi milioni 10
ikiwa ni msaada kwa mapacha hao wanne. Benki ya NMB imewafungulia
akaunti za watoto kwa kila mtoto na kuwawekea shilingi cha shilingi
milioni 10, kuwasaidia wazazi na watoto hao hapo baadaye. Wa pili kulia
ni mama mzazi wa mapacha hao, Sara Dimosso akiwa kabeba watoto wake huku
akisaidiwa na nduguye.
- Meneja
wa Benki ya NMB Tawi la Ubungo, Evelyne Mushi (kushoto) akimkabidhi
mama mzazi wa watoto wanne mapacha, Sara Dimosso (kulia) mfano wa hundi
ya shilingi milioni 10 ikiwa ni msaada kwa watoto mapacha wanne
aliojifungua hivi karibuni. Benki ya NMB imewafungulia akaunti za watoto
kwa kila mtoto na kuwawekea shilingi milioni 10 ikiwa ni kuwasaidia
wazazi na watoto hao hapo baadaye. Katikati ni baba wa watoto pacha
wanee, Abednego Andrew Mafuluka akishiriki kupokea msaada huo.
- Mama
mzazi wa watoto mapacha wanne, Sara Dimosso (kulia) pamoja na mume
wake, Abednego Andrew Mafuluka (katikati) wakipiga picha ya pamoja na
mfano wa hundi ya shilingi milioni 10 iliyokabidhiwa na Benki ya NMB
ikiwa ni msaada kwa watoto mapacha wanne aliojifungua hivi karibuni.
Kulia ni Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Ubungo, Evelyne Mushi mara baada
ya kuwakabidhi, Benki ya NMB imewafungulia akaunti za watoto kwa kila
mtoto na kuwawekea shilingi milioni 10 ikiwa ni kuwasaidia wazazi na
watoto hao hapo baadaye.
- Baadhi
ya maofisa wa Benki ya NMB wakiwa katika picha na familia ya Bwana na
Bibi Abednego Andrew Mafuluka pamoja na watoto wao mapacha wanne mara
baada ya kukabidhiwa mfano wa hundi ya msaada.
- Bwana
Abednego Andrew Mafuluka (katikati) akizungumza kuishukuru Benki ya NMB
baada ya kuguswa na kuamua kuwasaidia watoto wao mapacha wanne.
- Meneja
wa Benki ya NMB Tawi la Ubungo, Evelyne Mushi (kushoto) akizungumza
kuelezea namna Benki ya NMB ilivyoguswa na kuamua kuwasaidia watoto hao
mapacha wanne waliozaliwa pamoja.
- Mama
mzazi wa watoto mapacha wanne, Sara Dimosso (kulia) pamoja na mume
wake, Abednego Andrew Mafuluka akizungumza kuishukuru Benki ya NMB kwa
kuwasaidia shilingi milioni 10 iwawezeshe katika malezi ya watoto hao.
- Baadhi
ya maofisa wa Benki ya NMB wakiwa katika picha na familia ya Bwana na
Bibi Abednego Andrew Mafuluka pamoja na watoto wao mapacha wanne mara
baada ya kukabidhiwa mfano wa hundi ya msaada.
No comments:
Post a Comment