Na Godfriend Mbuya
Mwanaharakati wa Tanzania wa kupinga ndoa za utotoni,Rebeca Gyumi ambaye ni Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali, Msichana Initiative linalotetea
haki za wasichana kupata elimu amewataka vijana ambao wamepata nafasi ya kusoma
kuisaidia jamii katika mambo yanayowakwamisha kimaisha.
Gyumi ambaye ameshinda
tuzo ya umoja wa Mataifa inayotolewa kupitia UNICEF katika kipengele cha
mabadiliko ya kijamii ameyasema hayo katika kipindi cha SUPAMIX alipokuwa akielezea namna ambavyo ameweza kutambulika na kupewa tuzo na Shirika
la UNICEF kupitia Umoja wa Mataifa.
“Hakuna kitu kizuri kwangu kama kutumia elimu yangu kusaidia jamii ambayo
nimelelewa, mimi ni zao la jamii kuona kwamba elimu niliyopata kuna watu
walijinyima ili mimi niweze kusoma, ndiyo maana natumia nilichokipata kuweza
kurudisha angalau fadhila za jamii yangu” Amesema Gyumi.
Ghumi ameongeza kuwa ni vyema
viongozi ndani ya jamii yetu wakiwafundisha vijana namna ya kuitumikia
jamiii yetu kuliko vijana wa kitanzania kufundishwa na mataifa mengine juu ya
namna ya kuwa kiongozi bora ndani ya jamiii kwa kuwa jamii ya kitanzania
itaendelezwa na watanzania wenyewe .
Kutokana na ujasiri aliouonyesha wa kufungua kesi dhidi ya
serikali kuhusu sheria ya ndoa iliyokuwa inatoa fursa kwa mabinti wadogo
kuolewa ndipo UNICEF ikaweza kumtunuku tuzo ya kutambua mchango wake, shughuli
ambayo ilifanyika nchini Marekani.
No comments:
Post a Comment