Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo au Habari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejephotography Twitter @Fredynjeje
Mkurugenzi
Mkazi wa Shirika la kimataifa la Oxfam Nchini Tanzania Bw. Francis
Odokorachi akitoa neno la ufunguzi wakati wa uzinduzi wa
mradi wa kukuza utawala bora na uwajibikaji kupitia Teknolojia ya
kidijitali
Meneja
wa Programu ya Uwazi na Utawala Bora kutoka Oxfam Betty Malaki akieleza
kwa wadau(hawapo pichani) namna mradi huo utakavyofanya kazi na kuwa
umedhaminiwa na Serikali ya Ubelgiji ambao utawagusa zaidi wanawake na
vijana
Kefar Mbogela ambaye alikuwa muwezeshaji katika uzinduzi wa mradi huo wa kukuza utawala bora na uwajibikaji kupitia Teknolojia ya kidijitali akiendelea kutoa mwongozo
Mwakilishi
kutoka Ubalozi wa Ubelgiji Bw. Joris Becker akielezea sababu za
kuchagua Shirika la Oxfam kufanya nao mradi huo wa kukuza utawala bora
na uwajibikaji kupitia Teknolojia ya kidijitali
Mratibu
wa Mawasiliano ya kidijitali kutoka Oxfam Bill Marwa akielezea namna
teknolojia ya kidijitali itakavyotumika katika mradi huo.
Mmoja wa Muwasilisha Mada Bi. Maria Sarungi akielezea nguvu za mitandao ya kijamii na jinsi inavyoleta mabadiliko katika jamii.
Bwana
Richard Mabala kutoka TAMASHA akielezea kwa kina juu ya Uraghbishi
'Active Citizens' ili kuwapa uwelewa zaidi wadau ambao watahusika na
mradi huu wa kukuza utawala bora na uwajibikaji kupitia Teknolojia ya
kidijitali
Mwakilishi kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) akizungumzia shughuli mbalimbali zinazofanywa na mamlaka hayo.
Mwakilishi kutoka LHRC akizungumza mambo mbalimbali yanayohusu haki za Binadamu
Baadhi ya wadau wakitoa maoni na kuuliza maswali wakati wa uzinduzi wa Mradi huo
Picha zote na Fredy Njeje/ Blogs za Mikoa Tanzania
Shirika la Kimataifa la Oxfam Nchini Tanzania imezindua mradi wa miaka
miwili wenye nia ya kukuza utawala bora na uwajibikaji nchini kupitia
Teknolojia ya kidijitali.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Oxfam Tanzania Bw. Francis Odokorachi akitoa
maneno ya utangulizi katika uzinduzi wa mradi huo wa miaka miwili alisema mradi huo
utahusisha mikoa mine ambayo ni Geita, Arusha, Mtwara na Kigoma, ambao watapewa
simu 200 za kisasa ‘Smartphone’ ambazo zitatumika kutoa taarifa kiwa ajili ya kukuza
utawala bora na uwajibikaji nchini ,alisema
kupitia mradi huo wanatarajia kuwafikia watu 50 katika kila Mkoa.
"Watakaopatiwa simu hizo ni waraghibishi 200 waliokuwa
Katika mradi wa Chukua Hatua ambao watapatiwa mafunzo katika mradi
huo kuhusu sera, utawala bora, kuhusu wajibu wa wananchi na Serikali,"alisema Odokorachi.
Aliongeza kwamba kupitia teknolojia hii ya kidijitali itaongeza kasi ya
utawala bora lwa vijana na watu mbalimbali katika jamii ambapo katika mradi wa
Chukua Hatua ulikuwa ni mradi wa wananchi ambao walikuwa wakiibua mambo
mbalimbali katika maeneo waliopo kuhusu masuala ya kijamii, utawala bora,
ukatili wa kijinsia na mengineyo na viongozi kuweza kuchukua hatua katika
changamoto zilizokuwa zinaibuliwa.
Kwa Upande wake Meneja wa Programu ya Uwazi na Utawala Bora kutoka
Oxfam, Betty Malaki alisema mradi huo umedhaminiwa na Serikali ya Ubelgiji
ambao utawagusa zaidi wanawake na vijana.
“Matokeo ya mradi huo ni sauti za
wananchi kuhusu uwajibikaji na masuala mbalimbali kwa uharaka zaidi na
kuwafikia wengi kwa muda mfupi”. Alisema Malaki.
Naye Ofisa wa TCRA alisema kuongezeka kwa watumiaji wa mtandao nchini
kumewezesha kuwepo kwa matatizo ya kimtandao ikiwemo ulaghai na utapeli ambao
zaidi ni wizi wa fedha mtandaoni na mara nyingi simu na barua pepe hutumiwa
zaidi.
No comments:
Post a Comment