Social Icons

Friday 10 November 2017

SHIRIKA LA HIFADHI ZA TAIFA (TANAPA) SASA LAFIKILIA KUJA NA UTALII KWA BODA BODA NA BAJAJI


Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadi za Taifa ,(TANAPA) Pascal Shelutete akizungumza mara baada ya wageni hao kushuka baada ya kufanikiwa kufika kilele cha uHuru kwa kutumia Baiskeli.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

SHIRIKA la Hifadhi za Taifa (TANAPA) limesema litafikiria matumizi ya Boda boda na Bajaji kwa wageni watakao hitaji kutembelea Hifadhi zake endapo yatajitokeza maombi ya kutosha kuhusu matumizi ya vyombo hivyo.

Hatua hiyo inatokana na bidhaa mpya ya Utalii wa kutumia Baiskeli iliyoanzishwa hivi karibuni katika Hifadhi za Taifa za Mlima Kilimanjaro na Arusha kuanza kuwa kivutio kwa watalii kutoka nchi mbalimbali walioanza kufanya utalii wa Baiskeli.

Miongoni mwa watali hao ni pamoja na mpanda  milima mashuhuri Duniani kwa kutumia Baiskeli  ,Juanito Oiarzabal aliyeweka rekodi ya kuwa Mhispania wa kwanza kupanda Mlima Kilimanjaro huku akitumia saa 31 akiendesha baiskeli katika siku tano hadi kufika kilele cha Uhuru.

Juanito na wenzake wawili , Eduardo Pascuaz na Ramon Abecia waliianza safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa kutumia Baiskeli ,wakianza safari yao kupitia lango la Kilema ,aina hi ya utalii ikiwa ni bidhaa mpya katika Milima huo mrefu kuliko yote barani Afrika.
Aina hii mpya ya utalii ambayo kwa sasa imeanza kushika kasi katika Hifadhi za Taifa ,za Mlima Kilimanjaro,Arusha na Saadan inatokana na Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kuendelea kupanua wigo wa vivutio katika Hifadhi zake 16,
Meneja Mawasiliano na Mahusiano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete amesema hatua ya Juanito na wenzake kufika katika kilele cha Uhuru inaashiria kuanza kufunguka kwa aina hii mpya ya utalii katika Hifadhi za Taifa .
Shelutete amesema namna ambavyo Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) limekuwa mstari wa mbele katika kubuni aina mpya ya bidhaa za utalii ili  kushindana na nchi nyingine duniani katika uuzaji wa safari kwa watalii.
Kwa upande wake Juanito Oiarzabal ambaye amepata ulemavu wa kukatika vidole kutokana na barafu katika Milima mbalimbali aliyopanda amesema changamoto aliyokutana nayowakati wa kupanda mlima ni kuzoea hali ya hewa yam lima ambayo imekuwa ikibadilika kila mara.
Mkurugenzi wa kampuni ya Safari Bike Africa iliyoratibu changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa kutumia Baiskeli kwa wageni hao,Mario Martos amesema kampuni yake imekusudia kuleta mabadiliko katika sekta ya utalii kwa kufanikisha safari za watalii wa kutumia baiskeli.
Shirika la Hifdhi za Taifa (TANAPA) limejipanga kuhakikisha usalama wa hali ya juu kwa wageni watakaofanya aina hii mpya ya utalii katika Hifadhi zake kwa kuwa na taahadhari sambamba na waongoza wageni waliobobea katika kazi ya Utalii.

No comments: