Social Icons

Monday 22 January 2018

MBUNGE WA CHALINZE MH. RIDHIWANI KIKWETE AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO JIMBONI KWAKE

Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akimsikiliza Shedeli Mikole Mwenyekiti wa CCM kata ya Vigwaza wakati akiwa katika ziara ya kikazi kukagua huduma za maendeleo na miradi mbalimbali inayotekelezwa jimboni humo, Mh. Ridhiwan Kikwete ametembelea kata na vijiji vya Visezi, Buyuni , kata ya Vigwaza. na Magulumatari, Kisanga Kata ya Talawanda, Bago na Msinune kata ya Kiwangwa.
Sehemu ya Bidhaa zinazotengenezwa na vikundi vya Kimaendeleo. Kikundi cha Jipe Moyo ambacho ni moja kati ya vikundi vilivyofaidika na fursa za Mitaji Katika Halmashauri na Mfuko wa Jimbo ambao upo chini ya Mbunge wa Chalinze wakionyesha kazi zinazotokana na Mikono yao mbele ya Mbunge.
Mmoja wa wananchi akizungumza mbele ya Mh. Ridhiwani Kikwete mbunge wa jimbo la Chalinze .
Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akikagua Nguzo za umeme zipatazo 60 katika Kijiji cha Visezi. ambazo zipo hapo toka mwaka 2015 sasa ni miaka miwili toka Zilipoletwa hadi leo hazijaunganishwa. Serikali kupitia mradi wa Peri-Urban Enlightment Initiative watakuja waunganishia wananchi wa Visezi.
Baadhi ya wananchi wakiwa katika mkutano wa Mh. Ridhiwani Kikwete Mbunge wa jimbo la Chalinze.

No comments: