Social Icons

Monday, 14 May 2012

UGANDA YADAI KUMKAMATA KAMANDA WA NGAZI YA JUU WA LRA NA KUPATA MATUMAINI YA KUMKAMATA JOSEPH KONY



Jeshi  la  Uganda  limesema  kuwa  limemkamata kamanda  wa  ngazi  ya  juu  wa  kundi  la  wanamgambo  waasi wanaoongozwa  na  mbabe  wa  vita  Joseph Kony la  Lord’s Resistance Army LRA.
Kamanda  ametajwa kuwa ni Caesar Achellam (Pichani) ambapo wachunguzi  wa  mambo  nchini  Uganda wamesema  Achellam  alikuwa  sehemu  ya  uongozi  wa juu  wa  kundi  hilo  linaloongozwa  na  Kony  kuanzia miaka  ambayo  kundi  hilo  la  LRA  lilikuwa  likifanya shughuli  zake  kaskazini  mwa  Uganda.
Kundi la LRA lilianza shughuli  zake  dhidi  ya  serikali  ya  Uganda  katika  miaka ya  1980.
Kiongozi wa kundi hilo Bw. Kony  anatafutwa kwa  madai  ya  uhalifu dhidi  ya  binadamu.

No comments: