Social Icons

Sunday 10 February 2013

HUKU NDIKO TUNAPO ELEKEA KWA SASA: UTALII WA NGONO WASHAMIRI NCHINI..SOMA HAPA


Eneo la ufukweni mahali ambapo watalii wengi hupenda kupumzika 

KATIKA 

hali ya kawaida, tumezoea kuona watalii kutoka mataifa mbalimbali 
duniani wakija nchini kuangalia vivutio vya utalii vilivyopo.
Baadhi ya vivutio hivi ni Mlima Kilimanjaro, mbuga za wanyama, majengo ya kale, mapango na nyumba za kihistoria.

Hata 

hivyo, kumeibuka aina mpya ya utalii, unaojulikana kama utalii wa ngono,
ambao unashamiri kwa kasi ukihusisha zaidi watalii wanawake wanaofuata 
wanaume wa Kitanzania hasa vijana.

Uchunguzi

uliofanywa na Mwananchi Jumapili, unaonyesha kuwa utalii huo 
unaongezeka kwa kasi hasa katika maeneo yenye vivutio vingi vya utalii 
ikiwamo Arusha, Kilimanjaro na Zanzibar.

Imebainika

kuwa katika utalii huu, wanawake hasa watu wazima walio na umri kati ya
miaka 60 hadi 80 kutoka nchi mbalimbali, wamekuwa wakiingia nchini kwa 
lengo la kutafuta vijana wa kiume wa kustarehe nao.

Uchunguzi

huo unaonyesha kuwa wanawake ambao hawana vigezo vya uzuri 
vinavyopendwa na wanaume huko kwao, ikiwamo wembamba na urefu, husafiri 
kuja Tanzania kutafuta mwanamume atakayestarehe naye kingono.

Hali hiyo

inawakumba zaidi wanawake wanene, ambao kwa Ulaya hukosa wapenzi, hivyo
kulazimika kusafiri kuja Afrika Tanzania ikiwamo kutafuta mwenza wa 
kustarehe nao.

Uchunguzi

uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa, utalii huu umeshamiri nchini, 
ambapo vijana wa Kitanzania wanaufahamu na kukiri kuwa umewanufaisha na 
baadhi yao kuwasaidia kupata tiketi za kwenda kuishi Ulaya.

Katika 

Visiwa vya Zanzibar utalii huo unafanyika zaidi katika fukwe za Nungwi, 
Kiwengwa, Paje, Kendwa, Jambiani na maeneo mengine yaliyopo pembezoni 
mwa bahari.
Katika fukwe hizo vijana maalumu kwa kazi hiyo, wana kauli mbiu yao inayosema:“apewe mpaka apagawe, atoe tiketi.”

Kwa kauli

mbiu hiyo vijana hao wanamaanisha kuwa, kwa kila mwanamke 
watakayekutana naye, watatumia kila mbinu ili kumfurahisha hadi 
awasafirishe au kwenda naye Ulaya.

Abdulla 

Ali Haji (Sio jina halisi) ni miongoni wa vijana wanaojihusisha na aina 
hiyo ya utalii, akiishi visiwani humo ambapo anaeleza kuwa shughuli yake
kubwa ni kuzunguka katika fukwe mbalimbali akiwinda wanawake wa kizungu
wanaotaka kustarehe.
CHANZO DJ SEK BLOG

No comments: