Social Icons

Thursday, 7 November 2013

TUKIO KATIKA PICHA: SAFARI YA MWISHO YA MKE WA NDUGU YETU GREGORY MWANYIKA , MAREHEMU RITHA THOMAS KERARYO ALIYE FARIKI 03.11.2013 NA KUZIKWA 5.11.2013, WENGI WAMLILIA.

Ilikuwa ni Simanzi kubwa siku ambayo tulipatwa taarifa ya kushtushwa kuwa Ndugu yetu na jamaa yetu Mpendwa Ritha ametutoka....
Japo Taarifa ile ilikuwa ni ngumu kuamini lakini ukweli ukabaki kuwa ni kweli alikuwa amefariki Dunia.... 
Marehemu Alianza kusumbuliwa na kuumwa mnamo mwezi wa kwanza kwa tatizo la ini mpaka mauti ilipo mfikia tarehe 3.11.2013 ..
Kiukweli Mume wa Marehemu Bwana Gregory Mwanyika Binafsi nina mfahamu sana na hata alipo pata taarifa hizi za msiba alishindwa kuamini hadi siku ya tarehe 5.11.2013 alipo mwagia kaburini mchanga kwa mara ya mwisho...

Hivi ndivyo Safari yake ya mwisho ilivyo kuwa....

 
 Marehemu Ritha enzi za uhai wake

 Waombolezaji Mbalimbali wakiwa Msibani Kimara Stop over
 Rafiki wa Marehemu wakiwa wanawasili Msibani
 Mwili wa Marehemu ukiwa unawasili Nyumbani

 Mchungaji akiwa anasali na kutoa neno wakati wa ibada hiyo ya Mazishi nyumbani
 Waombolezaji wakiwa ndani

 Waombolezaji Ndugu jamaa na marafiki wakiwa wanasikiliza kwa umakini
Mume wa Marehemu Bwana Gregory Mwanyika akiwa katika Majonzi makubwa
 Wa kwanza kutoka kulia aliye kaaa ni Masache kasaka mmoja wa marafiki wakubwa wa marehemu akiwa na waombolezaji

 Jeneza la Marehemu Ritha

 Waombolezaji wakati wa ibada ya mazishi 

 Msemaji wa Familia akitoa Maelekezo
 Msemaji wa Familia akitoa wasifu wa Marehemu
 Shukurani zikitolewa
 Bwana Gregory Mwanyika Mume wa Marehemu Ritha aliye vaa shati jeusi akiwa katika mawazo na simanzi
 Mume wa Marehemu Bwana Gregory Mwanyika , akitoa Heshima za mwisho
 Bwana Masache kasaka akitoa salam za mwisho
 Baba wa Marehemu Ritha akitoa heshima za Mwisho kwa uchungu , huku akiwa amemshika Marehemu kwa Mara ya mwisho
 Mama wa Marehemu aliye vaa Nguo nyeupe akitoa Heshima za mwisho
 Dada wa Marehemu akitoa Heshima za Mwisho
 Mtoto wa Marehemu akitoa heshima za Mwisho
 Mchungaji alitoa Heshima za Mwisho
 Mume wa Marehemu Bwana Gregory Mwanyika akiwa katika Gari Maalum lililobeba Mwili wa Marehemu

 Safari ya Kuelekea makaburini maeneo ya kibanda cha mkaa
 Mume wa Marehemu wa kwanza kushoto Bwana Gregory Mwanyika  akiwa katika shughuli ya maziko
 Waombolezaji
 Safari ya mwisho inaelekea ukingoni
 Mchungaji akiliombea kaburi kabla ya kuzika
 Mwili wa Marehemu unaingizwa Kaburini
 Mwili wa Marehemu ukiwa kaburini
 Mtoto wa marehemu
 Mume wa Marehemu Bwana Gregory Mwanyika akiweka mchanga katika kaburi kabla ya kuanza kufukia
 Kazi ya kufukia kaburi inaanza
 Mume wa Marehemu Bwana Gregory Mwanyika akiweka taji la maua katika kaburi la Mke wake
 Wazazi wa Marehemu wakiweka Shada la Maua
 Dada wa marehemu akiweka shada la maua
  Mume wa Marehemu Bwana Gregory Mwanyika akiwasha mshumaa
 Marafiki wakubwa wa Bwana Gregory Mwanyika kutoka kulia ni Fredy Tony, Winfred Mbwilo  na Masache Kasaka ...
  Mume wa Marehemu Bwana Gregory Mwanyika akiwa na mwanae kaburini baada ya maziko
 Marafiki wa kubwa wa Marehemu na ambao alisoma nao zamani Mbalizi Sekondari huko mkoani Mbeya kutoka kushoto ni Fredy Tony, Masache Kasaka, Winfred Mbwilo na Elina Hongoli
 Tumerejea Nyumbani baada ya msiba...

Kwa Niaba ya wote ... na Blog hii tunawapa pole sana wafiwa Mungu azidi kuwapa nguvu hasa  Mume wa Marehemu Bwana Gregory Mwanyika  .


Imeandaliwa na kupigwa picha na Fredy Tony rafiki mkubwa wa Mume wa marehemu bwna Gregory Mwanyika.

BWANA AMETOA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.
AMEN




No comments: