Ikiwa una Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo au Habari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed
Gharib Bilal, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakijumuika na baadhi ya
biongozi wa Kitaifa na Waombolezaji, kushiriki katika shughuli ya kuagwa
mwili wa aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Marehemu Dkt.
Abdallah Kigoda, iliyofanyika leo Okt. 15, 2015 kwenye Viwanja vya
Karimjee jijini Dar es Salaam. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed
Gharib Bilal, akisalimiana na Mufti Mkuu wa Tanzania Abubakary Zubeiry,
wakati alipowasili kwenye Msikiti wa Maamur uliopo Upanga jijini Dar es
Salaam, leo asubuhi kwa ajili ya kuswalia mwili wa marehemu Dkt.
Abdallah Kigoda, aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, aliyefariki
dunia majuzi Hospitali ya Apollo nchini India, alipokuwa amelazwa
akitibiwa. Marehemu Kigoda anatarajia kuzikwa leo Jimboni kwake Handeni,
mkoani Tanga
Maafisa wa Bunge wakibebea Jeneza lenye mwili wa marehemu Dkt.
Abdallah Kigoda, wakati ulipowasili kwenye viwanja vya Karimjee jijini
Dar es Salaam, kwa ajili ya kuagwa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed
Gharib Bilal, akishiriki na baadhi ya Waumini wa dini ya Kiislamu,
kumswalia Marehemu Dkt. Abdallah Kigoda, aliyekuwa Waziri wa Viwanda na
Biashara, wakati wa swala hiyo iliyoswaliwa kwenye Msikiti wa Maamur
uliopo Upanga jijini Dar es Salaam, leo asubuhi. Marehemu Kigoda
anatarajia kuzikwa leo Jimboni kwake Handeni, mkoani Tanga
Sehemu ya waombolezaji na Wabunge waliohudhuria shughuli hiyo ya msiba Karimjee.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed
Gharib Bilal, akishiriki na baadhi ya Waumini wa dini ya Kiislamu,
kumswalia Marehemu Dkt. Abdallah Kigoda, aliyekuwa Waziri wa Viwanda na
Biashara, wakati wa swala hiyo iliyoswaliwa kwenye Msikiti wa Maamur
uliopo Upanga jijini Dar es Salaam, leo asubuhi. Marehemu Kigoda
anatarajia kuzikwa leo Jimboni kwake Handeni, mkoani Tanga
Baadhi ya Wanafamilia wa marehemu Dkt. Kigoda.
Spika wa Bunge Mama Anne Makinda, akizungumza kutoa salamu kwa niaba ya Bunge.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed
Gharib Bilal, akitoa heshima za mwisho mbele ya Jeneza lenye mwili wa
aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Marehemu Dkt. Abdallah Kigoda,
wakati wa shughuli ya kuagwa mwili huo iliyofanyika kwenye Ukumbi wa
Karimjee jijini Dar es Salaam, leo Okt. 15, 2015. Marehemu Kigoda
anatarajia kuzikwa leo Jimboni kwake Handeni, mkoani Tanga
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, akitoa heshima za mwisho mbele ya Jeneza
lenye mwili wa aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Marehemu Dkt.
Abdallah Kigoda, wakati wa shughuli ya kuagwa mwili huo iliyofanyika
kwenye Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, leo Okt. 15, 2015.
Marehemu Kigoda anatarajia kuzikwa leo Jimboni kwake Handeni, mkoani
Tanga.
No comments:
Post a Comment