Social Icons

Thursday 15 October 2015

UJENZI WA BARABARA YA JUU (FLY OVER) TAZARA DAR KUANZA;DK MAGUFULI ASHUHUDIA UTIAJI SAINI MKATABA‏

Ikiwa una Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo au Habari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com.

 Ramani ya Barabara ya Juu (Fly Over) itakavyokuwa baada ya ujenzi unaoanza mwezi ujao kukamilika Oktoba  2018. Mkataba wa ujenzi wa barabara hiyo utakaogharimu sh. bilioni 100 umesainiwa leo chini ya ushahidi wa Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli

 Waziri wa Ujenzi, ambaye pia ni Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk John Magufuli (aliyesimama katikati) akishuhudia utiaji wa saikni mkataba wa ujenzi wa barabara ya juu (Fly Over) katika makutano ya barabara za Mandela na Nyerere Tazara, Dar es Salaam leo. Wanaotia saini ni Meneja Mkuu wa Kampuni ya Sumitomo Mitsui itakayojenga barabara hiyo, Ichiro Aoki 9kushoto) na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara wa Serikali,Patrick  Mfugale. Ujenzi huo unaotarajia kuanza hivi karibuni  na kugharimu zaidi ya Bilioni 100 utakamilika Oktoba  2018. (PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA)




No comments: