Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @officialfredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
NAIBU
Kamishna wa Idara ya Uhamiaji, Abbas Irovya, akizungumza na waandishi
wa habari kuhusu idara hiyo kuanza kutoa hati kwa wageni wanaoingia
nchini kwa shughuli za muda mfupi, Makao Makuu ya Uhamiaji, Dar es
Salaam leo. Kulia ni Ofisa Vibali vya ukazi wa idara hiyo, Philon
Kyetema.
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
IDARA
ya Uhamiaji imeanzisha hati mbili ambazo zitatumika kwa wageni
wanaoingia na wanaotoka nje na kuondokana hati ya awali ya muda mfupi
(CTA).
Akizungumza
leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Msemaji Mkuu Idara ya
Uhamiaji, Naibu Kamishina Abbas Irovya amesema kuwa hati ya kwanza ni
ile ya muda atayeingia nchini kwa muda usiozidi siku 90 na baada hapo
anatakiwa kurudi alikotoka.
Naibu
Kamishina, Irovya amesema kuwa wanaoingia kwa ajili ya kutoa utalaam
wafanye hivyo kwa kuwa na hati hiyo na sio kuwa na ajira katika sehemu
hizo.
Amesema hati pili ni ile ile katika nchi zilizoingia makubaliano ya kutomia viza watatumia ya muda mfupi kwa kukaa kwa muda huo.
Aidha
ameesema wananchi watambue kuwepo kwa huduma hiyo ikiwa na kutoa
ushirikiano pale wanapowaona watu ambao wanatumia hati ya muda lakini
wanaendelea.
Irovya
amesema hati hizo mbili hazihusiani kwa wale wanaoingia nchini kwa
kutafuta ajira na wakitaka kufanya hivyo wanatakiwa kuomba kibali cha
kazi kutoka idara ya kazi.
No comments:
Post a Comment