Social Icons

Tuesday 26 January 2016

IDARA YA UHAMIAJI YAJA NA HATI MBILI ZA MUDA MFUPI KWA WAGENI.

Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @officialfredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
NAIBU Kamishna wa Idara ya Uhamiaji, Abbas Irovya, akizungumza na waandishi wa habari  kuhusu idara hiyo kuanza kutoa hati kwa wageni wanaoingia nchini kwa shughuli za muda mfupi, Makao Makuu ya Uhamiaji, Dar es Salaam leo. Kulia ni Ofisa Vibali vya ukazi wa idara hiyo, Philon Kyetema. 

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii 
IDARA ya Uhamiaji imeanzisha hati mbili ambazo zitatumika kwa wageni wanaoingia na wanaotoka nje na kuondokana hati ya awali ya muda mfupi (CTA).

Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Msemaji Mkuu Idara ya Uhamiaji, Naibu Kamishina Abbas Irovya amesema kuwa hati ya kwanza ni ile ya muda atayeingia nchini kwa muda usiozidi siku 90 na baada hapo anatakiwa kurudi alikotoka.

Naibu Kamishina, Irovya amesema kuwa wanaoingia kwa ajili ya kutoa utalaam wafanye hivyo kwa kuwa na hati hiyo na sio kuwa na ajira katika sehemu hizo.

Amesema hati pili ni ile ile katika nchi zilizoingia makubaliano ya kutomia viza watatumia ya muda mfupi kwa kukaa kwa muda huo.

Aidha ameesema wananchi watambue kuwepo kwa huduma hiyo ikiwa na kutoa ushirikiano pale wanapowaona watu ambao wanatumia hati ya muda lakini wanaendelea.


Irovya amesema hati hizo mbili hazihusiani kwa wale wanaoingia nchini kwa kutafuta ajira na wakitaka kufanya hivyo wanatakiwa kuomba kibali cha kazi kutoka idara ya kazi.

No comments: