Social Icons

Monday, 18 January 2016

MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA NCHINI AVIONYA VYAMA VYA SIASA KUACHA KUZUNGUMZIA SUALA LA MGOGORO ZANZIBAR

Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @officialfredynjejeblog Twitter @Fredynjeje

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Tanzania Jaji Francis Mutungi amevionya vyama vya siasa Tanzania Bara na Visiwani kuacha kuzungumzia suala la mgogogro wa Zanzibar kisiasa kwani suala hilo ni la kiserikali na tayari linafanyiwa kazi ya utatuzi kwa misingi ya haki za binadamu na sheria za nchi zinavyoelekeza.


Jaji Mtungi ametoa kauli hiyo leo Jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na wanahabari na kuwaonya wanasiasa na taasisi mbalimbali kuacha kuzungumzia mgogoro huo bila kuwa na ushahidi wa baadhi ya hatua zinazochukuliwa na serikali

Aidha Jaji Mutungi pia amewataka waandishi wa habari kuacha ushabiki wa vyama kwa kuandika habari za upande mmoja wa malalamiko kwani zinaweza kusababisha machafuko na kuhatarisha amani Visiwani Zanzibar.

Na Blogs za Mikoa

No comments: