Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @officialfredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
Raia wa Ujerumani (kulia) ambaye jina lake halikupatikana mara
moja, ametiwa na mbaroni na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa tuhuma za kutaka kuitoroka familia yake katika Hoteli ya Cate Dar es Salaam. Raia huyo alikuwa nchini na mkewe mwenye asili ya Afrika katika kipindi cha msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka. Alijaribu kumtoroka mkewe na mtoto (4) na kuwaacha wakidaiwa deni la sh. 315,000 baada ya kile kilichodaiwa kuzuka ugomvi baina yao.
Mtoto wao (4) akisaidiwa kupandishwa katika Gari
Raia wa Ujerumani huyo akitaka kuruka toka katika Gari la Polisi
Mke wa Raia wa Ujerumani wa pili kulia akiwa anaingia katika Gari kuelekea katika Kituo cha Polisi cha Msimbazi Dar es Salaam na wapili kulia ni kaka wa mwanamke wa Raia wa Ujerumani
Wananchi wakifuatilia kwa karibu tukio hilo
No comments:
Post a Comment