Social Icons

Monday, 18 January 2016

Wema Sepetu awafunda wabunifu chipukizi wa Lady In Red fashion show 2016

Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @officialfredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
DSC_0805

Mkurugenzi wa Fabak Fashions na mwandaaji wa onyesho la Lady in Red, Bi. Asya Idarous Khamsin (katikati) akimtambulisha rasmi mwanadada, Wema Sepetu (kushoto) ambaye ni miongoni mwa wadhamini wa Jukwaa hilo la Lady In Red 2016. (Kulia) ni Martin Kadinda ambaye naye miongoni mwa watendaji wanaoratibu jukwaa hilo. Onesho hilo linatarajiwa kufanyika 31 Januari ndani ya ukumbi wa Danken House uliopo Mikocheni jijini Dar es Salaam. (Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog).


DSC_0810

Mkutano huo wa utambulisho wa jukwaa la Lady Inn Red fashion show 2016 kama inavyoonekana pichani.

DSC_0808

Mwanadada Wema Sepetu akitoa nasaha zake kwa Wabunifu wa mavazi na wanamitindo (hawapo pichani) wakati wa utamburisho wa jukwaa la Lady In Red fashion show 2016 linalotarajiwa kufanyika 31 Januari.

DSC_0793

Martin Kadinda akitoa nasaha zake kwa wabunifu na wanamitindo waliojitokeza katika mkutano huo (hawapo pichani) kuhusiana na jukwaa la Lady In Red fashion show 2016.

DSC_0865

DSC_0903

Wabunifu wa mavazi na wanamitindo wakifuatilia mkutano huo wa utambulisho wa jukwaa la Lady In Red fashion show 2016.

DSC_0760

Baadhi ya wabunifu wa mavazi na mitindo wakifuatilia mkutano huo.

DSC_0881

DSC_0898

DSC_0873

DSC_0888

DSC_0885

DSC_0904

DSC_0765

DSC_0760

DSC_0902

DSC_0816

..Wakipata ‘selfie’ na Wema Sepetu

DSC_0833

..Wakipata ‘selfie’ na Martin Kadinda

DSC_0921

DSC_0830

Picha ya pamoja…

Nyota wa filamu za Bongo, ambaye pia aliwai kuwa Miss Tanzania kipindi cha nyuma, Wema Issac Sepetu ambaye pia ni mdhamini wa jukwaa la mitindo la Lady In Red fashion show 2016, Amewataka wabunifu wa mavazi na mitindo hasa chipukizi nchini kulitumia vizuri jukwaa hilo ili kufikia malengo yao.

Wema ameyasema hayo  alipokuwa akizungumza kwenye mkutano maalum uliowakutanisha Wabunifu wa mavazi na mitindo kwa lengo la kupanga mikakati ya ufanikishaji wake hiyo 31 Januari ambapo siku  hiyo onyesho hilo litafanyika ndani ya ukumbi wa Danken House uliopo Mikocheni jijini Dar es Slaam.

Wema Sepetu amewataka wabunifu hao kuja na utofauti wa kazi zao ambazo zitakuwa chachu na kivutio kwa watu hiyo itaongeza hali ya kukuwa kwa tasnia ya mitindo hapa nchini.

Naye Mkurugenzi wa Fabak Fashions na mwandaaji wa onyesho la Lady in Red, Bi. Asya Idarous Khamsin amebainisha kuwa, jukwaa hilo la Lady In Red litaendelea kuwapo kwani ni shule na daraja la Wabunifu wengi wa mavazi na mitindo ikiwemo kuibua chipukizi kila mwaka.

“Lady In Red fashion show 2016 ni ya kipekee na jukwaa hili ni fursa kwa kuinua wabunifu wa mavazi chipukizi kupata kuonekana zaidi na hata kukuza majina na ubunifu wao kujulikana ndani na nje” amefafanua Mama wa Mitindo, Asya Idarous.

Aidha, ameeleza kuwa, ilikutoa msisimko zaidi kwa jukwaa hilo, siku hiyo kutakuwa na mambo mbalimbaali zikiwemo ‘surprise’ kutoka kwa watu maalufu watakaokuwapo usiku huo.

Hadi sasa jukwaa hilo la Lady in red liimeweza kufikia mwaka wa 12  tokea kuanziashwa kwake limeweza kutoa wabunifu mbalimbali ambao kwa wengine wanamajina makubwa akiwemo Ally Rehmtullah, Martin Kadinda na wengine wengi ambao kwa sasa wamekuwa ni ‘icon’ ya jukwaa hilo.

Pia Asya Idarous ameomba wadau kujitokeza kuliiunga mkono onesho hilo la mavazi ikiwemo kudhamini ilikuongeza ukuaji wa tasnia hiyo hapa nchini.

Baadhi ya wadhamini waliopo kwa sasa ni pamoja na Fabak fashions, Wema Sepetu, Super News tv, Modewjiblog na wengine wengi.

Mo Blog

No comments: