Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
Na Walter Mguluchuma
Katavi yetu blog
Jeshi la Polisi Wilaya ya Mpanda linamshikilia John Noel Mkazi wa Mtaa wa Nsemlwa Manispaa ya Mpanda kwa tuhuma za kumchoma na moto mtoto wake wa kiume aitwaye Joji Noeri (4( viganja vyote viwili vya mikono yake na kumuuguza vibaya na kumsababishia kulazwa Hospitalini baada ya kumtuhumu kuwa amekomba mboga aina ya chainizi
Afisa ustawi wa jamii wa Hospitali ya Wilaya ya Mpanda Osca Mkenda aliwaambia waandishi wa Habari kuwa tukio hilo la unyanyasaji na ukatili lilitokea hapo juzi katika Mtaa wa Nsemlwa .
Alisema mtoto huyo aliyechomwa na moto na kuungua vibaya katika viganja vyake vya mikono yake yote miwili amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda katika wodi ya watoto namba 4 na alipokelewa haspitalini hapo hapo juzi.
Baba wa mtoto huyo ambae anashikiliwa na polisi anadaiwa kumchoma na moto mtoto wake huyo baada ya kumtuhumu kuwa amekomba boga aina ya chanizi zilizokuwa zimeandaliwa kwa ajiri ya mlo wa mchana .
Muuguzi wa wodi hiyo Joseph Mkangwa alisema hari ya mtoto huyo bado sio nzuri kutokana na majeraha makubwa ya moto aliyokuwa nayo ,
Alisema bado mtoto huyo anaendelea kupatiwa matibabu huku akiwa analelewa na bibi yake mzaa mama yake aitwaye Hdija Ally toka alipofikishwa hospitalini hapo.
Bibi wa mtoto huyo Hadija Ally alisema mjukuu wake alikuwa akiishi nyumbani na baba yake mzazi baada ya mama wa mtoto huyo kuwa wameachana na mume wake hapo mwaka jana .
Alisema inawezekana hata mke wake aliamua kuachana na kukimbia kwa mume wake kutokana na unyanyasaji kama huo walipokuwa wakiishi kama mume na mke na baada ya mke kuwa ameodoka ndipo mtoto huyo alilazimika kuishi na baba yake mzazi ambae amemtendea kitendo hicho cha kikatili na cha kusikitisha .
Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Mohamed
Rashid amekili kutokea kwa tukio hilo na alisema jeshi la polisi
linaendelea kumshiklia mtuhumiwa kwa mahojiano zaidi na atafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi utakapokuwa umekamilika .
No comments:
Post a Comment