Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
Waziri wa Fedha na
Mipango Dkt. Philip Mpango (katikati) akimkabidhi Mtendaji Mkuu wa Mahakama
Hussein Katanga (kushoto) mfano wa hundi wakati wa makabidhiano ya fedha hizo
mbele ya waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Naibu Katibu
Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju.
Waziri wa Fedha na
Mipango Dkt. Philip Mpango (katikati) akimkabidhi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya
Katiba na Sheria Amon Mpanju (kulia) mfano wa hundi wakati wa makabidhiano ya
fedha hizo mbele ya waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mtendaji
Mkuu wa Mahakama Hussein Katanga.
Waziri wa Fedha na
Mipango Dkt. Philip Mpango (katikati) akiongea na waandishi wa habari wakati wa
makabidhiano ya fedha zilizotolewa kwa Mahakama leo jijini Dar es salaam. Kulia
ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju na kushoto ni
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango (kushoto).
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria
Amon Mpanju (kulia) akitoa shukrani baada ya kupokea mfano wa hundi aliyopokea
kwa lengo la kusaidia mahakama leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Waziri wa Fedha
na Mipango Dkt. Philip Mpango.
Mtendaji Mkuu wa Mahakama
Hussein Katanga akitoa shukrani baada ya kupokea mfano wa hundi aliyopokea kwa
lengo la kusaidia mahakama leo jijini Dar es salaam. Katikati ni Katibu Mkuu
Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile na kulia ni Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango.
Baadhi ya waandishi wa
habari wakiendelea na kazi yao wakati wa makabidhiano ya fedha hizo mbele ya
waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.
(Na. Eleuteri
Mangi-Dar es
salaam).
Serikali imeikabidhi
Mahakama ya Tanzania kiasi cha Sh.bilioni 12.3 zilizoahidiwa na Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa Maadhimisho ya
Siku ya Sheria kwa lengo la kuiwezesha Mahakama kuimarisha utendaji kazi na kutekeleza
majukumu yake inapasavyo.
Akikabidhi fedha hizo mbele
ya waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam, Waziri wa Fedha na Mipango
Dkt. Philip Mpango amesema kuwa fedha zilizokabidhiwa kwa Mahakama ni mwitikio
wa kutekeleza ahadi ya Rais aliyoitoa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria
Duniani Januari 4, 2016.
“Ni matumaini ya
Serikali fedha hizo zitatumika vizuri na zitatumika kwa madhumuni
yaliyokusudiwa” alisema Dkt. Mpango.
Kwa upande wake Naibu
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju amemshukuru Mhe. Rais kwa
kwa kutekeleza ahadi aliyoitoa ndani ya siku nne na kuudhihirishia umma kuwa
kauli mbiu ya “Hapa Kazi Tu” anaisimamia kwa vitendo.
Naye Mtendaji Mkuu wa
Mhakama Hussein Katanga amesema kuwa fedha walizokabidhiwa zitasaidia ujenzi wa mahakama nchini na zipo
ndani ya bajeti ya mwaka 2015/2016 na watazitumia kulingana na malengo
yaliyokusudiwa.
No comments:
Post a Comment