Social Icons

Monday 22 February 2016

Mhe. Kairuki amsimamisha kazi mkuu wa chuo cha Utumishi wa Umma

Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje

Na. Lilian Lundo - Maelezo
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah  Kairuki amemsimamisha  kazi aliyekuwa mkuu wa chuo cha Utumishi wa Umma Said Nassoro kutokana na kushindwa kusimamia watumishi walioko chini yake
Mhe. Kairuki ametoa maamuzi hayo leo jijini Dar es Salaam  katika mkutano na waandishi  wa  habari katika moja ya kumbi zilizopo katika ofisi za Utumishi wa Umma.
“Namsimamisha Bwana Said Nassoro aliyekuwa mkuu wa chuo hiki kwa kushindwa kusimamia watumishi walioko chini yake  na kupelekea suala zima la usimamizi wa shughuli za chuo hususani katika matawi yake mbalimbali yaliyoko mikoani kuathirika,” alisema Mhe. Kairuku.
Mhe. Kairuki aliongeza kwa kusema kuwa usimamizi  wa Bw. Nassoro  ambao haukuwa wa ufanisi umetoa mwanya kwa viongozi mbalimbali wa matawi kufanya ubadhilifu wa mali za Umma ambapo mwaka  2011 na 2013 aliyekuwa mkurugenzi wa chuo upande wa tawi la Mtwara Silvanus Ngata aliongeza gharama za ujenzi.
Aidha taarifa kutoka Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) pamoja na TAKUKURU zilithibitisha ubadhilifu huo lakini mkuu huyo wa chuo hakuweza kuchukua hatua yoyote badala yake alimuhamisha Bw. Ngata kwenda kwenye tawi la Tabora na kuendelea na wadhifa wake.
Kutokana na ubadhilifu huo imempelekea Mhe. Kairuki  kumsimamisha kazi Bw. Ngata ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma tawi la Tabora na Bw. Joseph Mbwiro kutokana na matumizi mabaya ya fedha za malipo ya ada kiasi cha shilingi bilioni moja ambazo zilikuwa zikilipwa na wanafunzi kwa mwaka wa fedha 2014/15.
Mhe. Kairuki ameendelea kueleza kuwa  bado wanaendelea kuondoa watumishi wa Umma ambao hawafuati   mifumo na miongozo ya Utumishi wa Umma ili kuwabakiza  watumishi ambao wanaonyeshe taswira nzuri na kufuata mifumo na  miongozo  ya Utumishi wa Umma kwa ukamilifu wake.

No comments: