Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
Naibu
Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,
Mhe. Dk. Hamisi Kingwangalla mapema leo Februari 15, ametembelea kambi
ya Wagonjwa wa Kipindupindu pamoja na wale waliokumbwa na mafuriko
katika kijiji Mboliboli Kata Pawaga Wilayani Iringa ambapo hadi sasa
kambi hiyo ina wagonjwa 40 huku zaidi ya wagonjwa 223 walilipotiwa
kuugua tangu kipindupindu kimeanza katika eneo hilo.
Mkuu
wa mkoa wa Iringa Bi.Amina Masenza wakati wa kutoa taarifa yake kwa
Naibu Waziri Dk. Kigwangalla aliyetembea ya Mkuu wa mkoa huyo,
alimweleza kuwa kati ya wagonjwa hao 223, wagonjwa 17 ni watoto walio
na umri wa chini ya miaka 5, Mbali na hao hadi sasa yamesababisha kifo
kimoja.
Ugonjwa
huo umeelezwa kuwa umewakumba kutokana na mvua zilizonyesha na kubomoa
vyoo na kutapanya kinyesi hali iliyopelekea ugonjwa huo kusambaa Zaidi
katika makazi ya wananchi hao.
Hadi
sasa eneo hilo limekumbwa na maji huku wananchi wakilazimika kuyakimbia
makazi yao na hata kuzungukwa na maji karibu eneo kubwa na usafiri wa
watoa huduma kuwa wa shida ikiwemo kutumia boti maalum ama chopa.
Mkoa huo ulikumbwa na mvua mnamo Februari 3 hadi leo bado maji yameendelea kuzingira maeneo ya vijiji hivyo.
No comments:
Post a Comment