Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema
kwamba ameandaa mrithi wa shamba lake lakini sio mrithi wa Uganda na
Waganda watachagua mtu wa kuwaongoza pale ambapo yeye atastaafu wadhifa
huo.
Museveni ameyasema hayo kipindi ambapo
kampeni za lala salama zinaendelea nchini Uganda na uchaguzi wa kumpata
Rais wa nchi hiyo unafanyika siku ya alhamisi ya wiki hii.
Rais Museveni ambaye amedumu madarakani kwa
muda wa miaka 30 anatetea tena nafasi yake hiyo huku akijitamba kuwa
hakuna chama chenye uwezo wa kuweza kushinda chama chake cha National
Resistance Movement (NRM)
“Sidhani vyama vya upinzani vitashinda NRM.
Kwa sababu tunajua nguvu yetu. Tunajua tutashinda, lakini kama itakuwa
tumeshindwa basi tutawaachia wale ambao wameshinda. Lakini sidhani kuna
chama kinaweza kushinda NRM wakati huu,” amesema
Aidha kwa sasa katiba inaeleza umri wa juu
zaidi wa rais kuwa madarakani ni miaka 75. Kwa sasa Rais Museveni
anakaribia kutimiza umri wa miaka 72 maana kwamba mwaka wake wa mwisho
wa muhula ujao, iwapo ataingia madarakani, atakuwa na umri wa miaka 76.
No comments:
Post a Comment