Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
Bw Polepole akizungumza leo katika kongamano la shirikisho la wanafunzi wa Vyuo vya juu Iringa , shirikisho la CCM
Polepole akisalimiana na Diwani wa kata ya Nduli Bw Bashir Mtove
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Bw Richard Kasesela kushoto akiwa na Kamanda wa Uvccm Mkoa wa Iringa Bw Salim Asas
Na Matukiodaimablog
MWANAHAKATI
Humphrey Polepole amesema chama cha mapinduzi ( CCM) ni chama Chenye
misingi ya kweli ya kuwatumikia wananchi ukilinganisha na vyama vingine
asema Kazi ya kutumbua majipu ni nzuri
Huku
akiwataka wana CCM jimbo la Iringa Mjini kuanza Kazi ya kueleza mambo
mazuri yanayofanywa na Rais Dr John Magufuli katika utekelezaji wa
Ilani ya CCM.
Kuwa jimbo la Iringa halikuwa la kwenda mikononi mwa upinzani ataka viongozi wa CCM kujitathimini na kuona wapi walipoanguka.
Akizungumza
wakati wa ufunguzi wa kongamano la shirikisho la Vyuo vya elimu ya juu
la CCM Mkoa wa Iringa Bw Polepole alisema kuwa utendaji mzuri wa
serikali ya Dr Magufuli katika kutekeleza Ilani ya CCM umedhihirisha
wazi aina ya wana CCM ambao ni hazina na wanaweza kuleta maendeleo
makubwa katika jamii
Kwani
alisema kinachofanywa na Rais Dr Magufuli katika kuwatumikia watanzania
ni wazi kila Mwananchi anatambua sasa hazina kubwa iliyopo ndani ya
chama kwa kutokana na mazuri ambayo Serikali inafanya kazi.
Bw
Polepole alisema kuwa ni kweli CCM imepata ushindi katika uchaguzi mkuu
uliompa nafasi ya kwenda Ikulu Rais Dr Mahufuli japo alisema ushindi
huo wa asilimia 58 bado si mzuri wa kujivunia na kutaka nguvu iongezwe
zaidi ili kurudi katika ushindi wa asilimia 80 hadi 88
Alisema kuwa njia pekee ya kuongeza ushindi wa CCM ni lazima kufanya Kazi kukijenga chama na Kazi zake.
No comments:
Post a Comment