Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Watoto na Wazee Mhe. Ummy
Mwalimu akipokea vifaa kutoka kwa Mkurugenzi wa Bohari ya Dawa yaTaifa
Lauren Rugambwa Bwanakunu vitakavyotumika katika wodi ya Afya ya uzazi
ya Mama na Mtoto katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wa pili kushoto
ni Kaimu Mkurugenzi Hospitali ya Muhimbili Prof Lawerence Mseru na
nayefata ni katibu Mkuu wa wizara hiyo Mpoki Ulisubisya .
Mafundi wakifunga vitanda katika wodi mpya ya Afya ya uzazi ya
Mama na Mtoto katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Picha na raymond
Mushumbusi MAELEZOWaziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Watoto na Wazee Mhe. Ummy Mwalimu akielekezwa jambo katika nyaraka na katibu Mkuu wa wizara hiyo Mpoki Ulisubisya katika Kitengo cha Afya ya uzazi ya Mama na Mtoto katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Baadhi ya vijana wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na mfanyakazi wa Bohari Kuu ya dawa ya taifa (MSD) walishusha baadhi ya magodoro na vitanda vitakavyotumika katika wodi ya Afya ya uzazi ya Mama na Mtoto katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Watoto na Wazee Mpoki Ulisubisya akimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Bohari ya Dawa yaTaifa Lauren Rugambwa Bwanakunu wakati walipokuwa walisubiri kukabidhiana vifaa vitakavyotumika katika wodi ya Afya ya uzazi ya Mama na Mtoto katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Watoto na Wazee Mhe. Ummy Mwalimu akisaidiana na mmoja wa kijana wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kubeba boksi lenye takataka kwenda kuyatupa sehemu husika wakati wakifanya usafi katika jengo ambalo liliamriwa na Mhe Rais liwe wodi ya Afya ya uzazi ya Mama na Mtoto katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Watoto na Wazee Mhe. Ummy
Mwalimu akizungumza na Zuhura Abubakari mmoja ya wagonjwa waliohamishiwa
kwenye wodi mpya ya Afya ya uzazi ya Mama na Mtoto katika Hospitali ya
Taifa ya Muhimbili.
Na Raymond Mushumbusi MAELEZO
Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Watoto na Wazee Mhe. Ummy
Mwalimu amepokea vifaa vitakavyotumika katika wodi ya Afya ya uzazi ya Mama
na Mtoto katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ikiwa ni agizo la
Mhe.Rais alililolitoa mapema mwishoni wa wiki iliyopita katika
kuhakikisha kuwa wakinamama wanaojifungua hawalali chini.
Akipokea vifaa hivyo Mhe.
Ummy Mwalimu amesema anamshukuru sana Mhe Rais kwa kuona changamoto hii
ya wakina mama kulala chini wakati wakitoka kujifungua na kumuahidi
Mhe. Rais kusilimamia vyema suala hilo na kuwaagiza wakurugenzi husika
kumpa taarifa ya kuhusu vitanda na magodoro katika Hospitali zote zilizo
chini ya wizara yake.
“ Kuanzia sasa sitolala na natuma salamu kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya
kuwa fursa hii ni wajibu wao kutoa taarifa kuhusu maendeleo ya afaya
hasa katika vifaa hususan vitanda na magodoro ili kupunguza tatizo hili
la wagonjwa katika Hospitali zetu kulala chini wakati tuna uwezo wa
kupata vitanda na magodoro”
‘”Mhe.Rais amenifundisha na ametufundisha sote kwamba kutatua jambo sio mpaka mkae vikao au semina ili kujadili ila
inawezekana kama mkiweka nia ya kulifanya jambo hilo na kuachana na
zile kauli za tunalifanyia kazi, tupo katika michakato na kauli kama
hizo zisizotatua tatizo kwa wakati unaotakiwa”alisema Ummy.
Bohari ya Dawa ya Taifa imekabidhi jumla ya vitanda 120, Magodoro 120,
Mashuka 480, vitanda vya kuzalishia 10,vitanda 10 vya kulaza watoto
ambao hawajatimia Njiti na jumla ya vifaa vyote vina thamani ya shilling Million 100.
Uaandaaji wa wodi hiyo ya akimama wanaojifungua katika Hospitali ya
Taifa ya Muhimbili umekuja baada ya agizo la Mhe.Rais Dkt John Pombe
Magufuli alilolitoa hivi karibuni alipokuwa akiongea na wazee wa Mkoa wa
Dar es Salam na kutoa siku mbili kwa wizara Ya Afya kuhamisha ofisi
zilizokuwepo za kitengo Afya ya uzazi ya Mama na Mtoto na kuifanya kuwa wodi ya akina mama ili kupunguza tatizo la kulala chini kwa akina mama wanaotoka kujifungua.
No comments:
Post a Comment