Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
Na Walter Mguluchuma
Katavi yetu blog
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima amevuia kufanyika kwa maandamano ya wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu katika Kijiji cha Dilifu Kata ya Magamba Wilayani hapa waliotaka kuandamana kupiga kuzuiwa kunya shughuli katika eneo hilo na kupewa kampuni ya JANI INVESMET Inayomilikiwa na mwanasiasa mkongwe Crisanti Mzindakaya.
Wachimbaji hao wadogo wa madini ya dhahabu walikuwa wamepanga kufanya maandamano hayo hap oleo yaani jana kuanzia katika eneo hilo la Dilifu hadi katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mpanda umbali wa kilometa 13 kwalengo la kupinga uamuzi wa wizara ya Nishati na madini Kanda ya magharibu kwa uamuzi wake wa kuwataka wachimbaji hao kusitisha shughuli zao za uchimbaji katika eneo hilo na ipisha kampuni ya JANI INVESTMENT mali ya Mzindakaya.
Mkuu huyo wa Wilaya alilazimika hapo jana kwenda katika eneo hilo la Kijiji cha Dilifu na kufanya mkutano wa hadhara ilikuweza kuwasikiliza wachimbaji hao wadogo ambao walianza kujikusanya katika eneo hilo toka saa kumi na mbili asubuhi kwa ajiri ya kusubili mkutano huo wa hadhara.
Diwani wa Kata hiyo Philipo Kalyalya alieleza kuwa alieleza kuwa wachimbaji hao wadogo hao wapatao 2300 wanataka kupata ufumbuzi wa tatizo hilo kwani maisha yao ya kila siku yanategemea uchimbaji wa madini ya dhahabu katika eneo hilo.
Mwenyekiti wa chama cha wachimbaji wadogo wa madini wa Mkoa wa Katavi Wiliy Mbogo alisema kuwa wachimbaji wadogo wamekuwa wakikabiliwa na tatizo la ukosefu wa maeneo kutoka
na Wizara ya Nishati ya Madini kutowatengea maeneo ya kuchimba
wachimbaji wadogo kama ambavyo sheria ya madini inavyoeleza.
Alisema matokeo yake wizara hiyo imewapatia eneo wachimbaji wadogo katika eneo la Kijiji cha Kapalamenga yanakopatikana madini aina ya kopa wakati wachimbaji wengi wa madini wa Mkoa wa Katavi wanachimba dhahabu .
Mwenyekiti wa kitongoji cha Dilifu Ismaili Idd alieleza kwenye mkutano huo ambao wachimbaji walionekana kuwa na hasira kuwa eneo hilo ni eneo halali la Kijiji hivyo wawekezaji wanatakiwa kufuata taratibu .
Alisema hapo awali waliambiwa na Wizara ya Madini kanda ya magharibi kuwa eneo hilo wanalofanyia shughuli za uchimbaji ni eneo la kampuni ya uchimbaji ya madini ya GBA ambayo wao haajawahi kuiona hata siku moja kampuni hiyo .
Mwenyekiti huyo wa Kitongoji alieleza juzi walishangazwa na agizo kutoka Wizara ya madini kanda ya magharibi ikiwataka kuanzia leo yaani jana kusitisha shughuli zao za uchimbaji kwa kuwa eneo hilo wapewa kampuni nyingine inayoitwa JANI INVESTMENT inayomilikiwa na Crisanti Mzindakaya ndipo wachimbaji baada ya kupata taarifa hizo waliamua kufanya maandamano ya kupinga kwa kampuni hiyo kupewa maeneo.
Mussa Mkana mchimbaji mdogo alieleza kuwa karibu
maeneo yote ya uchimbaji wa madini kila wanapohitaji kupatiwa maeneo
hayo wamekuwa wanaambiwa kuwa yameisha chukuliwa na wachimbaji wakubwa
KIJANI INVESMENT hata hivyo maeneo hayo yamekuwa hayaendelezwi.
Daudi Sumuni alisema kikubwa wachimbaji wadogo hawaitaki kampuni hiyo kufanya shughuli kwenye eneo hilo na wao hawako tayari kuiona kwenye machimbo hayo ya dhahabu .
Kaimu Meneja wa madiwa wa kanda ya magharibi mhandisi Giliard Luyoka aliwataka wachimbaji hao wadogo kufanywa shughuli zao kwa kufuata sheria za uchimbaji wa madini .
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima aliagiza wachimbaji hao wadogo waendelee na shughuli zao za uchimbaji na sikama walivyokuwa wamezuia kufanya shughuli hiyo na akawahidi kurudi baada ya siku saba ilikuwapatia maekezo yatakayo kuwa yametolewa na waziri wa nishati na madini .
Alisema serikali inawahitaji sana wawekezaji lakini wafuate sheria na pia alisema yeye kama mkuu wa Wilaya hiyo haja pata taarifa yoyote ya kampuni hiyo kuomba eneo hilo
No comments:
Post a Comment