Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
akimwapisha Bw. Alphayo Kidata kuwa Kamishna
Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Na Raymond Mushumbusi- MAELEZO
15/3/2016. Dar es salaam.
Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
imekusanya takribani Sh. billioni 12 kutoka kwa wafanyabiashara ambao walikwepa
kodi na kupewa muda wa siku 14 na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kulipa kodi hizo kwenye mamlaka hiyo.
Akitoa takwimu hizo mara baada ya kuapishwa kuwa
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Alphayo Kidata amesema, kila
Mtanzania ana jukumu la kulipa kodi kwa mujibu wa sheria na sio kukwepa na amehaidi
kulisimamia vizuri suala la ukusanyaji wa mapato katika sehemu mbalimbali ili
kuongeza mapato ambayo yatasaidia kufanikisha maendeleo katika sekta
mbalimbali.
“Tutajitahidi kwa kila namna kuwaelimisha wananchi
wetu ili wafahamu wajibu wao na umuhimu katika kulipa kodi na sio kukwepa
kulipa kodi na tunawaomba wananchi kila waendapo kupata huduma yoyote ile iwe
katika sekta binafsi au Serikalini basi anatakiwa aombe stakabadhi za
manunuzi au huduma ili tuweze kudhibiti upotevu wa kodi” alisema Kidata.
Kamishna aliongeza kwamba Kidata mamlaka hiyo
ipo kwa ajili ya kuwahudumia wananchi na kama kuna suala lolote au tatizo
kuhusu kodi kuna ofisi katika mikoa yote ikiwa ni hatua ya kutatua shida zao na
kama kuna mtumishi yoyote wa mamlaka hiyo atashindwa kumuhudumia mwanachi
inavyotakiwa basi taarifa zitolewa mara moja kupitia namba zao zilizoko kwenye
tovuti ya mamlaka hiyo, ambayo ni www.tra.go.tz ili kuimarisha huduma zetu kwa
wateja.
Aidha Kamishna Mkuu huyo amesema kuwa
watawachukulia hatua wale wote ambao hawatalipa au hawajalipa kodi zao kwa
kuwapeleka mahakamani kwa kukaidi kulipa kodi halali kwa mujibu wa Sheria.
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeanzishwa kwa
mujibu wa Sheria na ina mamlaka ya usimamizi wa makusanyo ya Mapato Tanzania na
kwa kipindi cha hivi karibuni kumekuwa na ukwepaji wa kodi uliotokana na sakata
la upotevu wa makontena katika Bandari ya Dar es Salaam hivyo kuikosesha mapato
Serikali lakini jitihada thabiti zimefanywa na mamlaka hiyo kukusanya madeni
kutoka kwa wakwepa kodi na kuwafikisha mahakamani ambao wamekaidi kulipa.
No comments:
Post a Comment