Social Icons

Tuesday 15 March 2016

WAZIRI MKUU ATOA POLE KWA PROFESA ANNA TIBAIJUKA(MB) KWA KUFIWA NA MAMA YAKE

Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Kassim Majaliwa,akiweka saini katika kitabu cha maombolezo ya msiba wa mama wa Mbunge wa Muleba Kusini,Profesa Anna Tibaijuka, alipofika kutoa pole kwa wafiwa.Katikati ni Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Dk. Medard Kalemani na anayefuatia ni Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni ,ambao waliongozana na Waziri Mkuu kwenda kutoa pole kwa wafiwa.

 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Kassim Majaliwa(kulia),akimpa pole Mbunge wa Muleba Kusini,Profesa Anna Tibaijuka,ambaye amefiwa na mama yake.Waziri Mkuu yuko mkoani Kagera kwa ziara ya kikazi.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni(kulia),akimpa pole Mbunge wa Muleba Kusini,Profesa Anna Tibaijuka, aliyefiwa na mama yake,marehemu Aurelia Kajumulo.(Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)



No comments: