Social Icons

Tuesday 1 March 2016

Mahakama ya Tanzania yakutana na Wadau wa Haki jijini Dar es salaam, yasisitiza utoaji wa Haki kwa wakati.

Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje

 Mtendaji Mkuu wa Mahakama Bw. Hussein Katanga (katikati) akisisitiza jambo wakati wa kikao cha Mrejesho wa Wadau walioshiriki katika utoaji wa Elimu ya Sheria kwa wananchi  Februari 1 hadi 3, 2016 katika viwanja vya Mnazi mmoja,  jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mtendaji Mkuu Mahakama Kuu, Solanus Nyimbi na Kulia ni Msajili wa Mahakama ya Rufaa,  John Lugalema Kahyoza
 Mmoja wa washiriki wa kikao hicho akitoa mchango wake kuhusu uboreshaji wa huduma ya Mahakama.
 Msajili wa Mahakama ya Rufaa,  John Lugalema Kahyoza akizungumza na Wadau walioshiriki katika utoaji wa Elimu ya Sheria kwa wananchi Februari 1 hadi 3, 2016  katika viwanja vya Mnazi mmoja,  jijini Dar es salaam.
Washiriki wa kikao cha Mrejesho wa Wadau walioshiriki katika utoaji wa Elimu ya Sheria kwa wananchi  Februari 1 hadi 3, 2016 katika viwanja vya Mnazi mmoja, wakifuatilia kikao hicho leo jijini Dar es salaam.
Picha na 4. Mmoja wa washiriki wa kikao hicho akichangia.


Na. Aron Msigwa – Dar es salaam.

Mahakama ya Tanzania imesema kuwa inaendelea na mkakati wa kufanya maboresho ya miundombinu yake ili kurahisisha  utoaji wa huduma ya mahakama kwa wadau na wananchi kwa wakati.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Mtendaji Mkuu Mahakama ya Tanzania Bw. Hussein Katanga wakati wa kikao cha Mrejesho wa Wadau walioshiriki katika utoaji wa Elimu ya Sheria kwa wananchi Februari 1 hadi 3 mwaka huu katika viwanja vya Mnazi mmoja,  jijini Dar es salaam.

Bw. Katanga amewaambia wadau hao kuwa Mahakama ya Tanzania inaendelea kufanya mabadiliko ya huduma zake kutokana na ushirikiano mkubwa inaoupata kutoka Serikalini pia kutoka kwa wadau wa Haki wanaoiwezesha Mahakama kufanya maboresho hayo kwa lengo la kukuza Utoaji wa Haki nchini.

Amesema ili kusogeza huduma karibu na wananchi  Mahakama itatekeleza Mpango mkakati wa miaka 5 wa kuiwezesha kushirikiana kwa karibu zaidi na wadau na Taasisi za utoaji Haki katika masuala yanayohusu shughuli za kila siku za utendaji wa Mahakama nchini.

“ Mahakama tutaanzisha mpango wa miaka 5 ambao utaanzisha mfumo wa wa kushirikiana na wadau wetu kwa karibu katika mambo yanayohusu shughuli zetu ili kuwaondolea wananchi usumbufu na upotevu wa muda pindi wanapofuatilia huduma” Amesema.

Amefafanua kuwa Mahakama imeshaanza kujenga majengo mapya ya kisasa ya Mahakama za Mwanzo katika maeneo mbalimbali  nchini ikiwemo Mahakama ya mwanzo Kigamboni jijini na Kawe zote za jijini Dar es salaam, Mahakama ya Wilaya ya Mkuranga  na Kibaha mkoani Pwani ili kurahisisha utoaji wa Haki.

“ Mahakama sasa tuko katika mwelekeo mzuri wa kufanya mabadiliko, kwa kushirikiana na wataalam wetu wa ndani wakiwemo Chuo Kikuu Ardhi , tunaendelea kujenga majengo mapya ya Mahakama katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Mahakama ya Mwanzo Kigamboni, Mkuranga, Kibaha na Kawe ambayo yatakamilika ifikapo Juni mwaka huu” Amesisitiza.

Bw. Katanga ameongeza kuwa mpango uliopo ni kuhakikisha kuwa majengo yaliyopo yanakarabatiwa sanjali na ujenzi wa majengo mapya katika Mahakama zote 133 nchi nzima.

Aidha, amebainisha kuwa Mahakama inaendelea kujenga mazingira wezeshi kwa watumishi wake ikiwemo ununuzi wa mabasi ya kusafirishia watumishi, magari madogo na Pikipiki ili kuwawesha watumishi wa Mahakama kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Mahakama Kuu Solanus Nyimbi akizungumza na wadau hao amewataka wafanye kazi kwa kushirikiana katika kuwahudumia wananchi ili kuongeza imani yao kwa Mahakama.

Amezitaka Taasisi na wadau wanaohusika na utoaji wa Haki kujikita katika kushughulikia matatizo ya wananchi ili kufanikisha dhana ya Utoaji Haki kwa Wakati ili kwenda na mpango uliowekwa na Mahakama wa kuondoa mrundikano wa mashauri mahakamani na ule wa kuzifuta kesi zilizokaa muda mrefu.

Naye Msajili wa Mahakama ya Rufaa,  John Lugalema Kahyoza ametoa wito kwa Taasisi za Utoaji wa Haki kukutana mara kwa mara ili kujdili na kutatua changamoto zinazoukabili Utoaji wa Haki nchini.


No comments: