Social Icons

Wednesday 30 March 2016

WAZIRI UMMY MWALIMU AWAKEMEA WANAOJICHUKULIA SHERIA KWA WATUMISHI WA AFYA

Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje

Ummy Mwalimu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akizungumza na na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula kufuatia tukio la mmoja wa Madaktari kupigwa na mwananchi. Kulia ni Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Kambi.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akemea tabia inayotaka kujengeka ndani ya jamii ya kuwashambulia watumishi wa afya hasa Madaktari na Wauguzi.
Amevitaka vyombo ya dola kuwachukulia hatua wananchi wanaojihusisha na vitendo hivi ambavyo vitaathiri utoaji wa huduma za afya kwa wananchi hasa wa kipato cha chini.
Mhe Ummy amewasili Mtwara jana akiongozana na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Kambi ambapo alifanya mazungumzo na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula.
Amewaonya wananchi kutoitumia vibaya dhamira ya dhati ya Rais Dkt. John Magufuli na Serikali ya kuimarisha nidhamu na uwajibikaji katika utumishi wa umma kwa kujichukulia sheria mkononi.
Ummy Mwalimu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akizungumza na mmoja wa wazee aliyefika kupata matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula mara baada kuwasili hospitalini hapo kuzungumza na wafanyakazi.
Ummy Mwalimu
Ummy Mwalimu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akizungumza na baadhi ya wananchi waliokusanyika nje ya hospitali kufuatia tukio la mwananchi kumpiga daktari.
Ummy Mwalimu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akisikiliza maoni kutoka kwa mmoja wa wananchi aliyefika hospitalini hapo.
Ummy Mwalimu
Mh. Ummy Mwalimu akizungumza na na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula kufuatia tukio la mmoja wa Madaktari kupigwa na mwananchi. Kulia ni Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Kambi.
Ummy Mwalimu
Baadhi ya watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula wakimsikiliza Mh. Ummy Mwalimu (hayupo pichani).
Ummy Mwalimu
Mh. Ummy Mwalimu akisikiliza hoja mbalimbali za madktari wa hospitali hiyo.
Ummy Mwalimu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akikagua neti ya mmoja wa mama aliyejifungua katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula.
Ummy Mwalimu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akifurahi kumuona mmoja wa watoto aliyezaliwa katika wodi ya wazazi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula mara baada ya kufanya mazungumzo na watumishi wa hospitali hiyo.
IMG-20160329-WA0058
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akifurahi jambo na mmoja wa kina mama alipotembelea wodi ya wazazi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula.
Ummy Mwalimu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akizungukia baadhi ya maeneo ya hospitali hiyo.

No comments: