Aliingia moja kwa moja na mteja wake ndani na kufunga
mlango, akapandisha kimini chake hadi usawa wa tumbo na kujilaza kitandani
akimsikilizia mteja wake naye asaule. Hakutaka kufanya kosa kama la yule mzee
wa mwanzo akadai hela yake mapema na kupewa kama walivyokubaliana.
Yule jamaa alionekana mzoefu wa biashara hiyo na alionekana
anahamu kweli na hilo lilionekana wazi kwa jinsi mlingoti wake ulivyosimama.
Moyoni Joy alifurahia wateja wa aina ya yule kaka kwa sababu hakuwa wa kupoteza
muda kwenye kale kamchezo kwa sababu hata haikupita dakika mbili yule jamaa
alikuwa tayari amefika kileleni.
Baada ya kumaliza, yule jamaa alisimama na kupandisha
suruali yake aliyoishusha wakati wa kale kamchezo kachafu. Wakati wanavaa
masikio ya Joy yalikuwa makini akasikia kishindo cha kitu kwenye sakafu ya kile
chumba.
Alipotazama aligundua waleti ikiwa chini ya uvungu wa kile
kitanda, akasimama na kuibana kwa mguu huku akimsubiri yule mteja wake aondoke
.
Alipoondoka, haraka akaichukua ile waleti na kufungua ndani
yake. Ama kweli mlango mmoja ukifunga mwingine unafunguka. Ndani ya ile waleti
kulikuwa shilingi laki mbili taslimu.
Akazificha kwenye matiti yake na kutoka nje haraka, ili
asije kukutana na yule jamaa akiwa ameshtuka kama amepoteza fedha zake.
Haya ndiyo yalikuwa maisha ya machangudoa wote hapo
kijiweni; siku unakosa, siku unapata. siku unadhurumiwa, siku unadhurumu.
Alisimama na kuchukua upande wa khanga na mkoba wake kutoka
kwenye kilinge cha ‘babu’(mmiliki wa gesti) na kujifunga vizuri, hiyo ikiwa ni
kuhitimisha kazi yake aliyoifuata usiku huo ambayo iliisha mapema kweli kwa
sababu wenzake ndiyo kwanza walikuwa wakianza kazi.
Alichukua kila kitu chake na kupanda bajaji, haraka
akiondoka eneo hilo kuelekea mtaani kwake, maeneo ya Tandale. Hakika zari
lilimdondokea kiasi kwamba fedha ambazo angepaswa kuzipata kwa kuzihangaikia
kwa siku tatu au nne alizipata kwa usiku mmoja tu.
Akamshukuru Mungu wake, akashuka salama na kwenda moja kwa
moja kuugonga mlango wa chumba chake, lakini kulikuwa kimya. Akafungua busati
la mlango wake na kupapasa chini akachukua ufunguo na kuingia ndani akawa
amewahi kabla ya shoga yake, Batuli ambaye muda wake wa kurudi ni saa 10 za
usiku.
Wote wawili walikuwa wamepanga ndani ya nyumba hiyo kwa
kuchangia chumba kimoja, ni marafiki wa tangu utotoni na wote wametokea Dodoma
na kukimbilia Dar kwa sababu ya ugumu wa maisha, mwenzake kazi zake ilikuwa ni
kuuza baa huku yeye akiuza mwili.
Kabla usingizi haujampitia aliamua kupekua tena ile waleti
yake ili atazame vitu vingine vilivyosalia mle ndani, akagundua kitambulisho
cha yule mwanaume jina lake likiwa ni Joseph Gabriel. kimeandikwa CRDB Azikiwe
Branch Manager yaani meneja wa tawi la Azikiwe benki ya CRDB.
Akakagua tena, akagundua business card ambayo ndani yake
kulikuwa na namba zake za simu na mawasiliano mengine. Akahakikisha hamna kitu
tena. Akaviweka vile vitu juu ya dressin tebo na kulala.
Itaendelea wala usikose
No comments:
Post a Comment